Omega

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kigiriki
Herufi za kawaida
Α α Alfa 1 Ν ν Ni 50
Β β Beta 2 Ξ ξ Ksi 60
Γ γ Gamma 3 Ο ο Omikron 70
Δ δ Delta 4 Π π Pi 80
Ε ε Epsilon 5 Ρ ρ Rho 100
Ζ ζ Dzeta 7 Σ σ ς Sigma 200
Η η Eta 8 Τ τ Tau 300
Θ θ Theta 9 Υ υ Ipsilon 400
Ι ι Iota 10 Φ φ Phi 500
Κ κ Kappa 20 Χ χ Khi 600
Λλ Lambda 30 Ψ ψ Psi 700
Μ μ Mi 40 Ω ω Omega 800
Herufi za kihistoria1
Digamma 6 San 90
Stigma 6 Sho 90
Heta 8 Koppa 90
Sampi 900
1 Viungo vya Nje:
Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje

Omega, yaani "o kubwa" (Ω ω) ni herufi ya ishirini na nne pia ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.

Jina la Kigiriki lamaanisha "O kubwa" kwa kuitofautisha na Omikron au "O ndogo". Maana matamshi ya omega ilikuwa "oo" (o ndefu).

Alama yake ilikuwa pia na maana ya namba 800.

Katika sayansi omega hutumiwa hasa kama alama ya omu (Ohm) yaani kipimo cha ukinzani wa umeme.

Omega ikiwa herufi ya mwisho ya alfabeti ya Kigiriki, hutumiwa mara nyingi kwa kutaja mwisho. Hivyo ni kinyume cha mwanzo au alfa.

Usemi wa Biblia hujulikana kuhusu Mungu kuwa "Alfa na Omega, mwanzo na mwisho" (Ufunuo wa Yohane 21:6).