Theta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kigiriki
Herufi za kawaida
Α α Alfa 1 Ν ν Ni 50
Β β Beta 2 Ξ ξ Ksi 60
Γ γ Gamma 3 Ο ο Omikron 70
Δ δ Delta 4 Π π Pi 80
Ε ε Epsilon 5 Ρ ρ Rho 100
Ζ ζ Dzeta 7 Σ σ ς Sigma 200
Η η Eta 8 Τ τ Tau 300
Θ θ Theta 9 Υ υ Ipsilon 400
Ι ι Iota 10 Φ φ Phi 500
Κ κ Kappa 20 Χ χ Khi 600
Λλ Lambda 30 Ψ ψ Psi 700
Μ μ Mi 40 Ω ω Omega 800
Herufi za kihistoria1
Digamma 6 San 90
Stigma 6 Sho 90
Heta 8 Koppa 90
Sampi 900
1 Viungo vya Nje:
Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje

Theta ni herufi ya nane katika Alfabeti ya Kigiriki. Theta kubwa Θ ina umbo la "O" yenye mstari wa katikati. Theta ndogo θ ina umbo la duaradufu nyembamba pamoja na mstari lala wa katikati lakini kuna pia umbo lisilofungwa kama ϑ.

Kwa matumizi ya tarakimu inamaanisha namba 9.[1]

Matamshi yake siku hizi ni sawa na "th" kwa Kiswahili.

Matumizi ya kisayansi[hariri | hariri chanzo]

Jinsi ilivyo kawaida na herufi mbalimbali za kigiriki inatumiwa kama kifupi kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hesabu na sayansi. Mifano kadhaa ni

  • katika fani ya fizikia
    • Theta ndogo θ au ϑ ni alama ya halijoto
    • Theta ndogo ni alama kwa kiwango cha pembe katika usokotaji.
    • Theta kubwa Θ hutumiwa kama alama ya kuonyesha nguvu ya uga magnetiki
  • katika fani ya astronomia
    • Theta kubwa Θ inataja saa za nyota
    • Theta ndogo ϑ hutaja nyota inayoonekana kwenye nafasi ya tisa katika kundinyota kulingana na nguvu ya nuru yake.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Theta ina maana ya tisa ingawa siku hizi ni herufi ya nane. Sababu yake ni ya kwamba alama ya digamma imepotea katika alfabeti lakini imebaki kama tarakimu ya sita