Mkoa wa Bonde la Ufa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mikoa ya Kenya
Mkoa wa Bonde la Ufa
Rift Valley Province
Mahali pa Mkoa wa Kati
Makao Makuu Nakuru
’‘‘Mji Mkubwa’’’ Nakuru
Eneo

- Jumla
Nafasi ya 1 kati ya mikoa ya Kenya
182,413 km²
Wakazi


 - Jumla (2007)  - Msongamano wa watu / km²
Nafasi ya 1 kati ya mikoa ya Kenya
7,630,300
42/km²
Lugha mkoani Kikalenjin
Kimaa
Kikuyu

Mkoa wa Bonde la Ufa ni mkubwa kati ya mikoa minane ya Kenya. Umepakana na Sudani, Ethiopia, Uganda na Tanzania, halafu na mikoa ya Magharibi, Nyanza, Mashariki, Kati na Pwani. Jina latokana na Bonde la Ufa linalopita katika mkoa.

Eneo la mkoa ni 173,854 km² kuna wakazi karibu milioni saba (6,987,036 mwaka 2000). Umbo lake ni kanda ndefu linalounganisha watu wwenye maisha na utamaduni tofauti sana. Makao makuu ya mkoa yapo Nakuru.

Ndani ya mkoa kuna maeneo yenye rutba sana lakini pia nchi yabisi hata jangwa. Maziwa makubwa ya magadi ni tabia mojawapo wa mkoa huu kama vile Ziwa Turkana, Ziwa Nakuru au Ziwa Naivasha.

Watu wa mkoa wa Bonde la Ufa ni wa makabila mengi. Wenyeji ni wafugaji kama Wamassai au Samburu au wakulima kama sehemu kubwa ya Wakalenjin ambao ni kundi la makabila yaliyo karibu kiutamaduni. Kundi kubwa ni Wakalenjin.

Wakinamama wa Pokot walio Wakalenjin

Idadi ya wakazi huongezeka haraka. 1989 palikuwa na wakazi milioni 4.9, 1999 tayari na wakazi milioni 6.9 na kadirio la 2007 ni milioni 8.8.

Mwenye kaskazini ya mkoa kunwa wakimbizi wengi kutoka Sudan katika kambi kubwa la Kakuma.

Wilaya za Mkoa wa Bonde la Ufa[hariri | hariri chanzo]

Wilaya (Makao Makuu):

  1. Baringo (Kabarnet)
  2. Bomet (Bomet)
  3. Buret (Litein)
  4. Kajiado (Kajiado)
  5. Keiyo (Iten / Tambach)
  6. Kericho (Kericho)
  7. Koibatek (Eldama Ravine)
  8. Laikipia (Nanyuki)
  9. Marakwet (Kapsowar)
  10. Nakuru (Nakuru)
  11. Nandi (Kapsabet)
  12. Narok (Narok)
  13. Samburu (Maralal)
  14. Trans Mara (Kilgoris)
  15. Trans-Nzoia (Kitale)
  16. Turkana (Lodwar)
  17. Uasin Gishu (Eldoret)
  18. Pokot Magharibi (Kapenguria)