Udhu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu ya mfululizo wa makala juu ya

Uislamu

Imani na ibada zake

Umoja wa Mungu
Manabii
Misahafu
Malaika
Uteule
Kiyama
Nguzo za Kiislamu
ShahadaSwalaSaumu
HijaZaka

Waislamu muhimu

Muhammad

Abu BakrAli
Ukoo wa Muhammad
Maswahaba wa Muhammad
Mitume na Manabii katika Uislamu

Maandiko na Sheria

Qur'anSunnahHadithi
Wasifu wa Muhammad
Sharia
Elimu ya Sheria za KiislamuKalam

Historia ya Uislamu

Historia
SunniShi'aKharijiyaRashidunUkhalifaMaimamu

Tamaduni za Kiislamu

ShuleMadrasa
TauhidiFalsafaMaadili
Sayansi
SanaaUjenziMiji
KalendaSikukuu
Wanawake
ViongoziSiasa
Uchumi
UmmaItikadi mpyaSufii

Tazama pia

Uislamu na dini nyingine
Hofu ya Uislamu

Udhu katika lugha ya Waislamu inamaanisha uzuri na usafi.

Sheria inawadai kutumia maji kwenye viungo maalumu kwa nia ya kujitwahirisha.

Ufafanuzi[hariri | hariri chanzo]

Kutawadha ama ni lazima ama inapendekezwa.

a. Ni lazima kutawadha kwa mambo matatu:

1. Kuswali: Katika Kurani Mwenyezi Mungu anasema: "Enyi Mlioamini! Mnaposimama kwa ajili ya swala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni" [5: 6]

2. Kutufu Alkaba: Kwa kauli yake Mtume Mohamed kumwambia mwanamke aliye katika hedhi: "Usitufu mpaka utwahirike" (imepokewa na Bukhari).

3. Kushika Msahafu: Kwa neno lake Mwenyezi Mungu: "Hawaigusi isipokuwa wale waliotwahiriwa" [56: 79]

b. Kutawadha kunasuniwa katika mambo mengine yasiyokuwa hayo:

Kwa neno lake Mtume alisema: "Hajilazimishi na udhu isipokuwa mwenye imani" (imepokewa na Ahmad).

Kunapendekezwa zaidi kutawadha wakati wa kujadidisha udhu kwa kila swala, kutawadha kwa kumtaja Mwenyezi Mungu na kuomba, wakati wa kusoma Qur’ani, kabla ya kulala, kabla ya kuoga, na kutokana na kumbeba maiti na baada ya kila tukio la kutangua udhu, hata kama hataki kuswali.

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.