Remigius wa Reims

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Remiji wa Reims)
Mt. Remigius akimbatiza Clovis I, mchoro wa Master of Saint Gilles, 1500 hivi (National Gallery of Art, Washington, D.C.)
Sanamu ya Mt. Remigius huko Simpelveld, Uholanzi.

Remigius au Remi wa Reims, (kwa Kifaransa: Rémi au Rémy; Cerny-en-Laonnois, karibu na Laon, Picardy, 437Reims, Champagne, 13 Januari 533) alikuwa askofu wa Reims (Ufaransa) kwa miaka zaidi ya 60.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1][2].

Mafanikio[hariri | hariri chanzo]

Alipata umaarufu kama mtume wa Wafaranki kwa sababu alileta kwa Kristo kabila hilo kubwa la Kigermanik, la kwanza kujiunga na Kanisa Katoliki bila kupitia kwanza Uario. Tarehe 25 Desemba 496 alimbatiza mfalme Clovis I na kwa njia hiyo alivutia Wafaranki wengi katika Ukristo, jambo muhimu sana katika historia ya Kanisa na ya Ulaya kwa kuwa hilo lilikuwa kabila la kwanza la Wagermanik kuingia Kanisa Katoliki bila kupitia Uario halafu lilitawala sehemu kubwa ya Ulaya magharibi na kuunda ustaarabu wake.

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Kati ya maandishi yake, mengi yamepotea[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Great Synaxaristes: Kigezo:Gr icon Ὁ Ἅγιος Ρεμίγιος Ἐπίσκοπος Ρημῶν. 13 Ιανουαρίου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.
  2. January 13 Archived 12 Oktoba 2011 at the Wayback Machine.. The Roman Martyrology.
  3. Few authentic works of Remigius remain: his "Declamations" were elaborately admired by Sidonius Apollinaris, in a finely turned letter to Remigius, but are now lost. Cfr. Book IX, p. vii. Four letters survive: one containing his defence in the matter of Claudius, two written to Clovis, and a fourth to Bishop Falco of Tongeren. Cfr. Philip Schaff, "The New Schaff-Herzog Encyclopedia of Religious Knowledge," entry by A. Hauck

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.