Odilo wa Cluny

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Odilone katika Basilika la Mt. Urban, Troyes, Ufaransa.

Odilo wa Cluny (962 hivi - 1 Januari 1049) alikuwa abati wa tano wa monasteri ya Kibenedikto ya Cluny nchini Ufaransa, ambaye aliifanya kuwa muhimu kuliko zote za Ulaya na kuhamasisha urekebisho wa nyingine nyingi.

Mkali kwake mwenyewe, alikuwa mpole na mwenye huruma kwa wengine; kwa jina la Mungu alipatanisha mataifa yaliyokuwa yanapigana, wakati wa njaa alitegemeza kwa hali na mali wanyonge. Pia alianzisha kumbukumbu ya Marehemu Wote siku iliyofuata sikukuu ya Watakatifu Wote[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Januari[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Martyrologium Romanum
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.