Cluny

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abasia ya Cluny mwaka 2004.

Abasia ya Cluny (au Cluni, au Clugny), ilikuwa monasteri ya Wabenedikto, maarufu kwa kuongoza urekebisho wa utawa na wa Kanisa lote kuanzia karne ya 10.

Ilijengwa kwa mtindo wa Kiroma katika eneo la Burgundy, leo mkoa wa Saône-et-Loire, Ufaransa.

Mwanzilishi wake, William I wa Aquitania, mwaka 910 alimteua Berno wa Cluny awe abati wa kwanza, chini ya Papa Sergius III tu. Hivyo alionyesha njia ya kukwepa watawala wasiendelee kuingilia vyeo vya Kanisa kwa malengo yao ya kisiasa na ya kiuchumi badala ya yale yaliyokusudiwa ya kidini.

Monasteri nyingine nyingi zilifuata njia hiyo na kivyo kuinua hali ya kiroho ya utawa na wa Kanisa kwa jumla katika karne zilizofuata.

Mwaka 1790, wakati wa Mapinduzi ya Kifaransa, abasia iliporwa na kubomolewa kwa kiasi kikubwa.

Coat of Arms of Cluny Abbey: "Gules two keys in saltire the wards upwards and outwards or overall a sword in pale argent".

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Bainton, Roland H.. The Medieval Church. Princeton: D. Van Nostrand Company Inc.,

1962.

  • Conant, Kenneth J. (1968). Cluny. Les églises et la maison du chef d'Ordre.
  • Cowdrey, H. E. J. (1970). The Cluniacs and the Gregorian Reform.
  • Evans, Joan (1968). Monastic Life at Cluny 910-1157. Oxford: Oxford University Press.
  • Lawrence, C. H. (1984). Medieval Monasticism.
  • Marquardt, Janet T. (2007) From Martyr to Monument: The Abbey of Cluny as Cultural Patrimony.
  • Mullins, Edwin (2006) In Search of Cluny: God's Lost Empire.
  • Rosenwein, Barbara H. (1982). Rhinoceros Bound: Cluny in the 10th Century.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Coordinates: 46°26′03″N 4°39′33″E / 46.43417°N 4.65917°E / 46.43417; 4.65917

Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Cluny kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.