Nenda kwa yaliyomo

Musa wa Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Musa wa Roma (alifariki Roma, Italia, 251) alikuwa padri wa Roma ya Kale aliyeongoza jimbo baada ya kifodini cha Papa Fabiani wakati wa dhuluma ya kaisari Decius.

Aliona vema kupatanisha na Kanisa wale ambao waliwahi kukana imani ya Kikristo na kwa wakati huo walikuwa wagonjwa na katika hatari ya kufa. Akikaa gerezani muda mrefu aliwafariji mara nyingi kwa kuwashirikisha maneno ya barua za Sipriani mfiadini, askofu wa Karthago [1].

Hatimaye akafa gerezani [2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakristo wa madhehebu mbalimbali kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Novemba[3].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  • Agostino Amore, Mosè, presbitero, santo, martire di Roma, in Bibliotheca Sanctorum, vol. IX, pp. 649-650
  • Hippolyte Delehaye, Étude sur le légendier romain : les saints de novembre et de décembre, Bruxelles, 1936, p. 49
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.