Mtindo wa Kigothi mamboleo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanisa kuu la Mtakatifu Yosefu, Dar es Salaam.
Kanisa la Mitume Petro na Paulo huko Ostend (Ubelgiji), lililojengwa miaka 1899-1908.

Mtindo wa Kigothi mamboleo (kwa Kiingereza: Gothic Revival architecture, Victorian Gothic, neo-Gothic, au Gothick) ulikuwa mtindo wa usanifu majengo ambao uliiga kwa kiasi tofauti ule wa Kigothi uliotawala Ulaya katika karne za kati.

Mtindo huo ulianza Uingereza mwishoni mwa miaka ya 1740, ulistawi mwanzoni mwa karne ya 19, na kutawala katika ustaarabu wa Magharibi katikati ya karne hiyo.

Mfano maarufu katika Afrika Mashariki ni kanisa kuu la Mt. Yosefu (kwa Kiingereza: St Joseph Cathedral church) jijini Dar es Salaam, Tanzania, lililojengwa kwa umahiri na wamisionari Wabenedikto kutoka Ujerumani kuanzia mwaka 1897 hadi 1902[1] likatabarukiwa mwaka 1905.[2]. Hadi sasa ni kanisa kuu la Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Kati ya sifa zake, mojawapo ni vioo vya rangi nyuma ya altare[3].

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Michael Hodd, East Africa Handbook: The Travel Guide, p. 344
  2. (Kiitalia) St. Benedict Monastery Archived 2012-08-02 at Archive.today
  3. St. Joseph's Cathedral at Lonely Planet

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

  • Christian Amalvi, Le Goût du moyen âge, (Paris: Plon), 1996. The first French monograph on French Gothic Revival.
  • "Le Gothique retrouvé" avant Viollet-le-Duc. Exhibition, 1979. The first French exhibition concerned with French Neo-Gothic.
  • Hunter-Stiebel, Penelope, Of knights and spires: Gothic revival in France and Germany, 1989. ISBN|0-614-14120-6
  • Phoebe B Stanton, Pugin (New York, Viking Press 1972, ©1971). ISBN|0-670-58216-6
  • Summerson, Sir John, 1948. "Viollet-le-Duc and the rational point of view" collected in Heavenly Mansions and other essays on Architecture
  • Sir Thomas G. Jackson, Modern Gothic Architecture (1873), Byzantine and Romanesque Architecture (1913), and three-volume Gothic Architecture in France, England and Italy (1915)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons