Mont Blanc

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mont Blanc

Mont Blanc (yaani "Mlima Mweupe" kwa Kifaransa; kwa Kiitalia: Monte Bianco) ni mlima mkubwa wa Alpi wenye kimo cha mita 4,810 juu ya usawa wa bahari. Iko kwenye mpaka wa Italia na Ufaransa ikiwa nchi hizo mbili hazikubaliani kilele kiko upande gani.

Mont Blanc hutajwa mara nyingi kama mlima mkubwa wa Ulaya lakini hii inategemea kama Elbrus katika Kaukazi inahesabiwa upande wa Asia au upande wa Ulaya.

Jina la mlima limetokana na theluji na barafu za kudumu zilizopo juu yake. Mitelemko ya mlima imefunikwa na barafu yenye unene wa mita 28. Barafuto za Mont Blac zafikia chini pande zote mbili katika Ufaransa na Italia katika mabonde yenye makazi ya watu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mont Blanc kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.