Nenda kwa yaliyomo

Lambati wa Maastricht

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Lambati alivyouawa.

Lambati wa Maastricht (pia: Lambert, Lambertus, Lambrecht, Lambaer, Baer; Maastricht, leo nchini Uholanzi, 636 hivi – Liege, leo nchini Ubelgiji, 705 hivi [1]) alikuwa askofu wa Tongeren-Maastricht, kati ya Ubelgiji na Uholanzi kuanzia mwaka 670 hadi kifodini chake.

Alipopelekwa uhamishoni aliishi miaka saba katika monasteri ya Stavelot. Aliporuhusiwa kurudi jimboni[2], alifanya uchungaji kwa sifa njema.

Akishirikiana na Wilibrodi aliinjilisha kwa bidii eneo hilo, alimsaidia Landrada kuanzisha monasteri ya kike na alimlea Hubati wa Liege, mwandamizi wake [3].

Hatimaye aliuawa na wapinzani wake akiwa na Petro na Audolet, watoto wa ndugu yake waliojaribu kumlinda, labda kwa sababu alimlaumu mtawala kwa uzinifu wake [4].

Tangu kale wote watatu wanaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama watakatifu wafiadini[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 17 Septemba[6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "Lambert of Maastricht", Ökumenisches Heiligenlexicon
  2. Albers, Petrus Henricus. "St. Lambert." The Catholic Encyclopedia Vol. 8. New York: Robert Appleton Company, 1910. 26 August 2017
  3. http://www.santiebeati.it/dettaglio/92911
  4. ""Prince Bishop St. Lambert", Province-de-Liège". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-06-12. Iliwekwa mnamo 2024-06-03.
  5. Wasyliw, Patricia Healy. Martyrdom, Murder, and Magic: Child Saints and Their Cults in Medieval Europe, Peter Lang, 2008, p. 81ISBN 9780820427645
  6. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.