Kisiwa cha Krismasi
Territory of Christmas Island Kisiwa cha Krismasi | |
![]() | |
Lugha rasmi | Kiingereza, Kichina, Kimalay |
Makao makuu | Flying Fish Cove |
Utawala | Eneo la ng'ambo la Australia |
Gavana | Michael Jeffery |
Pesa | Dollar ya Australia |
Wimbo wa taifa | Advance Australia Fair |
![]() |
Kisiwa cha Krismasi ni eneo dogo la Australia katika Bahari Hindi takriban 500 km upande wa kusini ya Jakarta mji mkuu wa Indonesia na 2,400 km kaskazini ya Australia yenyewe.
Kuna wakazi 1,600 wanokalia vijiji katika kaskazini ya kisiwa. Theluthi mbili za eneo lake ni hifadhi la taifa kwa sababu ya mazingira yake ya pekee pamoja na mimea na wanyama wake wasiopatikana mahali pengine duniani.
Jina na Historia[hariri | hariri chanzo]
Jina lake liliteuliwa kwa sababu nahodha Mwingereza William Mynors aliyekuwa kati ya watu wa kwanza wa kuona kisiwa hiki alifika hapa siku ya Krismasi mwaka 1643. Wakati ule kisiwa kilikuwa bila watu.
Katika karne zilizofuata kisiwa kilitembelewa mara chache kwa sababu mwambao wake ni vigumu kukaribia kwa jahazi kubwa. Lakini baada ya kugunduliwa fosfeti kisiwani migodi ikaanzishwa na wafanyakazi kupelekwa hapa kutoka Singapur, China na Malaysia.
Hawa walikuwa mababu wa wenyeji wa leo. 1958 kisiwa kikakabidhiwa kwa Australia.
Mazingira[hariri | hariri chanzo]
Kiswiwa cha Krismasi ni mahali pa pekee kwa sababu kinaonekana hakikutembelewa na watu hadi karne ya 16 na hakukukaliwa na watu hadi mwishow a karne ya 19. Hivyo spichi nyingine zimehifadhiwa zilizoharibiwa penginepo.
Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]
- Christmas Island Shire official website
- Christmas Island Act 1958 Archived 18 Desemba 2008 at the Wayback Machine.
- Christmas Island katika Open Directory Project
- Christmas Island Archived 25 Desemba 2018 at the Wayback Machine. in the CIA World Factbook