Kipanya wa Rudd

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kipanya wa Rudd
Kipanya wa Rudd
Kipanya wa Rudd
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Rodentia (Wanyama wagugunaji)
Nusuoda: Myomorpha (Wanyama kama panya)
Familia: Muridae (Wanyama walio na mnasaba na panya)
Nusufamilia: Deomyinae (Wanyama wanaofanana na vipanya-miiba)
Thomas, 1888
Jenasi: Uranomys
Dollman, 1909
Spishi: U. ruddi
Dollman, 1909

Kipanya wa Rudd (Uranomys ruddi) ni mnyama mgugunaji mdogo na spishi pekee ya jenasi Uranomys wa nusufamilia Deomyinae katika familia Muridae aliye na nasaba karibu na vipanya manyoya-magumu.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Kipanya huo ana ukubwa zaidi kuliko vipanya wa kawaida. Urefo wa mwili ni sm 8.4-13.4 na urefu wa mkia ni sm 5.3-7.9. Uzito ni g 41-53. Manyoya kwenye mgongo ni magumu kama yale ya vipanya manyoya-magumu lakini siyo kama yale ya vipanya-miiba. Upande wa juu na mbavu zina rangi ya kahawa na upande wa chini ni mweupe. Miguu imefunikwa kwa manyoya meupe.

Kipanya wa Rudd hujulikana kupitia msambao mkubwa katika Afrika kusini kwa Sahara, pamoja na angalau Kenya, Tanzania na Uganda katika Afrika ya Mashariki, lakini kamwe wako wengi. Kwa kawaida hukamatwa katika makazi ya savana. Anafikiriwa kukiakia usiku na hula wadudu hasa.