Aroni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Haruni)
Aroni
Ibada kwa ndama wa dhahabu ilivyochorwa na Nicolas Poussin.

Aroni (au Harun; kwa Kiebrania: אַהֲרֹן, ′aharon; kwa Kiarabu: هارون, Hārūn, kwa Kigiriki: Ἀαρών, Aaron; alifariki juu ya Mlima Hor, leo nchini Yordani, karne ya 13 KK) alikuwa kaka wa Musa. Dada yao aliitwa Mariamu.

Walikuwa watoto wa Amram na wa shangazi yake Jokebed, wote wa kabila la Lawi, taifa la Israeli.

Ndiye aliyepakwa mafuta na Musa kuwa kuhani mkuu wa kwanza wa dini yao, na makuhani wote waliofuata walitakiwa kuwa wanaume waliotokana naye kwa kuzaliwa upande wa baba[1].

Wanae waliitwa Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Julai[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Aberbach, Moses and Leivy Smolar. "Aaron, Jeroboam and the Golden Calves." Journal of Biblical Literature 86 (1967): 129-140.
  • Ginzberg, Louis. The Legends of the Jews. Translated by Henrietta Szold and Paul Radin. 7 vols. Philadelphia: Jewish Publication Society of America, 1909-1938.
  • Kaufmann, Yehezkel. The Religion of Israel. Translated by Moshe Greenberg. New York: Schocken Books, 1960.
  • Kennett, R.H. "The Origin of the Aaronite Priesthood." The Journal of Theological Studies 6 (Januari 1905): 161-186.
  • "Aaron", McCurdy, J. F. and Kaufmann Kohler. Jewish Encyclopedia. Funk and Wagnalls, 1901–1906; which cites
  • Meek, Theophile James. "Aaronites and Zadokites." The American Journal of Semitic Languages and Literatures 45 (Aprili 1920): 149-166.
  • Meek, Theophile James. Hebrew Origins. Rev. ed. New York: Harper & Brothers, 1950.
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Aroni kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.