Gaudensi wa Rimini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanduku linalotunza masalia yake.

Gaudensi wa Rimini (Efeso, leo katika Uturuki, 280 hivi - Rimini, Italia, 14 Oktoba 360 BK) anakumbukwa kama askofu wa kwanza wa Rimini (Italia Kaskazini), aliyewajibika nyakati za dhuluma.

Wazazi wake walikuwa Wakristo waliomsomesha vizuri, ila wakaja kuuawa na wafuasi wa Mani. Hapo alihamia Roma (308) alipopata ubatizo halafu upadri (332) na uaskofu (346) akatumwa Rimini.

Huko, pamoja na maaskofu wa jirani alipinga uzushi wa Ario, mbali ya ibada za Upagani. Hatimaye aliuawa na Waario walioungwa mkono na kaisari[1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Oktoba[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/90632
  2. Martyrologium Romanum
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.