Gairo
Kata ya Gairo | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Mkoa | Morogoro |
Wilaya | Gairo |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 33,209 |
Gairo ni jina la makao makuu ya Wilaya ya Gairo katika Mkoa wa Morogoro, Tanzania yenye Postikodi namba 677000.
Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012, kata ya Gairo ilikuwa na wakazi wapatao 33,209, wengi wao wakiwa Wakaguru. [1] Gairo ni mji mkubwa na kata ya kiutawala katika Wilaya ya Gairo katika Mkoa wa Morogoro, Tanzania, Afrika Mashariki[2].
Ipo kwenye barabara kuu ya Dodoma hadi Dar es Salaam na ni kituo cha kupitisha mizigo, pamoja na kituo cha kusafirisha mazao ya kilimo cha wilaya hiyo.
Kufikia 2002, idadi ya wakazi wa mji ilikuwa 16,982,[3]
Kikabila, watu wengi ni Wakaguru.
Maendeleo[hariri | hariri chanzo]
Gairo ni mmojawapo kati ya miji ambayo inakua sana nchini na unajulikana kwa kuwa unazalisha mazao ya biashara na chakula kama vile viazi vitamu, mahindi, maharagwe na vilevile kwa ufugaji.
Kutokana na ukaribu wake na barabara kuu ya Dodoma, mji wa Gairo umekuwa kati ya walishaji wakubwa kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.
Hapo zamani Gairo ilikuwa chini ya jimbo la uchaguzi la Kilosa, baadaye ulipata kuwa jimbo linalojitegemea.
Mnamo Machi 2012 umefanywa wilaya.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2015-03-22.
- ↑ https://en.wikipedia.org/wiki/Gairo,_Tanzania#cite_note-TCRA-Morogoro-1
- ↑ "Gairo, Tanzania", Wikipedia (in English), 2021-07-16, retrieved 2023-05-14
![]() |
Kata za Wilaya ya Gairo - Mkoa wa Morogoro - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Chagongwe | Chakwale | Chanjale | Gairo | Idibo | Iyogwe | Kibedya | Mandege | Msingisi | Nongwe | Rubeho | Chigela | Italagwe | Leshata | Madege | Magoweko | Mkalama | Ukwamani |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Morogoro bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Gairo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa na viongozi wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |