Chuo Kikuu cha Kikristo cha Pan Africa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Chuo Kikuu cha Kikristo cha Pan Africa (PAC) ni chuo kikuu cha Kikristo mjini Nairobi, Kenya. Taasisi hii ina utambuisho rasmi kamilifu na ni chuo kikuu cha binafsi ambacho kina katiba, kilichoidhinishwa na Tume ya Kenya ya Elimu ya juu, na kuidhinishwa na serikali ya Kenya kutuza shahada za digrii.

Historia[hariri | hariri chanzo]

PAC ilianzishwa na mdhamini wake mkuu, Pentecostal Assemblies of Canada(PAOC), na ilianza shughuli zake mwaka wa 1978 kama chuo ya Bibilia. Kama shirika la utume mwongofu(mission-minded), PAOC ilianza kuwatuma wamishenari katika nchi nyingi za Afrika katika miaka za 1920. Matokeo ya juhudi zao yalikuwa uibukaji wa kanisa za Taifa nchini Kenya na nchi jirani. Barani, makanisa haya kwa ujumla yanajulikana kama Pentecostal Assemblies of God (PAG). Kupitia juhudi za wachungaji, wamishenari na wainjilisti, baadhi ya fellowships za PAG zimekuwa zaidi ya makanisa 3000.

Nairobi, na sehemu yake ya kati na upatikanaji, ilikuwa chaguo la mahali pa PAC. Ukumbi upande wa kaskazini-mashariki nje ya mji mkuu ulipatikana mwaka wa 1978, na ulinunuliwa kwa ajili ya uanzishwaji wa taasisi ya kupeana shahada.

Madarasa ya PAC ilifunguliwa mnamo 2 Mei 1978, ikiwa na wanafunzi 6 na idadi hiyo imeongezeka na kuwa zaidi ya wanafunzi 300. Kitivo cha PAC kinajumuisha raia wa Afrika na vilevile walilmu wasio Waafrika walioletwa na PAOC. Kwa kuongezea Kitivo cha kufunza wanafunzi siku nzima, Chuo hiki Kikuu kina idadi ya kitivo ambacho si cha siku nzima katika Nyanja zao za utaalam. . Kitivo cha siku nzima kwa kawaida huwa kina uzoefu wa kichungaji na digrii ya waliopata shahada.

Mwaka wa 1985, Tume ya Elimu ya Juu (Commission of Higher Education-CHE) ilianzishwa ili kuendeleza elimu ya chuo kikuu nchini Kenya, na hasa katika uratibu wa mipango ya muda mrefu, maendeleo ya wafanyakazi, udhamini na maendeleo ya kimwili wa vyuo vikuu nchini Kenya. Katika msingi huu, CHE iliiandikisha PAC kama chuo kikuu mwaka wa 1989. Tangu wakati huo, PAC imekuwa ikifanya kazi na CHE ikielekea utambulisho rasmi na Wizara ya Elimu. Mitaala ya PAC kwa ajili ya shahada zinazotolewa ulipitishwa rasmi na CHE kuanzia mwaka wa 2006.

Chuo kikuu cha kikristo cha Pan Africa lilituzwa rasmi katiba tarehe 15 Februari 2008 na Mwai Kibaki,Rais wa Kenya. PAC ikawa tisa chuo kikuu cha kibinafsi cha 9 kupewa katiba nchini Kenya.

Maelezo mafupi[hariri | hariri chanzo]

Faili:Pac faculty staff.jpg
PAC wafanyakazi na Kitivo yao mbele ya jengo admin

Kwa kuwa ni chuo kikuu cha kimataifa, PAC huwafunza wanafunzi kutoka nchi nyingi ndani na nje ya Afrika. Wanafunzi wengi wa kitambo waliohitimu (alumni) wa PAC wanashiriki katika mafunzo ya taasisi ya Biblia kufundisha, huduma ya uchungaji, uongozi wa dhehebu, kazi za kimishenari na wizara ya para-kanisa. Kila mwaka, idadi ya alumni wa PAC huendeleza masomo yao ya uzamili katika vyuo vikuu na seminari duniani kote.

Kaulimbiu[hariri | hariri chanzo]

The Leadership University: Character, Service, Transformation

Misheni[hariri | hariri chanzo]

Kuendeleza viongozi wa Kikristo, kuongeza wafuasi Yesu Kristo ambao wamejiami kumtumikia Mungu, kanisa na jamii zao huku wakiimarisha na kuzidisha waumini katika Afrika na duniani kote

Maono[hariri | hariri chanzo]

Kuwa chuo kikuu cha Kikiristo kinachoongoza cha kuchagua barani Afrika, na sifa ya elimu ya hali ya juu na elimu ya utaalamu katika jamii ya kujifunza na huduma, ambayo ni chombo muhimu katika mabadiliko ya jamii.

Maadili makuu[hariri | hariri chanzo]

  • Kutafuta ukweli na uadilifu
  • Kuisisitiza umuhimu wa watu
  • Heshima na kushirikiana kwa anuwai ya jamii ya PAC
  • Kipaumbele na kuzingatia malezi ya kiroho na kibibilia
  • Umuhimu ya mafunzo katika maudhui, muundo na mchakato
  • Ubora katika kufanya kazi, kutembea na huduma ya kiroho miongoni mwa wanafunzi, Kitivo na wafanyakazi
  • Kufunza maadili ya uongozi miongoni mwa wanafunzi, Kitivo na wafanyakazi

Masomo[hariri | hariri chanzo]

PAC kinataka kupanua ushawishi wake kwa kuendeleza programu zake za masomo zinazoshughulikia mahitaji muhimu katika nyanja zote za jamii na msukumo wa mabadiliko kupitia Kristo unaozingatia utauwa uongozi. PAC sasa ina programu zifuatazo:

Bachelor of Business Leadership

Bachelor of Business Leadership inalenga kuendeleza kwa mwanafunzi mtazamo wa kikristo kuelekea uongozi wa ushirika wa biashara. Programu hii inajumuisha mafunzo ya Uongozi unaozingatia falsafa ya uongozi wa mtumishi kwa maeneo nne yanayodhuru.

  • Uhasibu na Fedha
  • Elimu ya soko
  • Usimamizi wa rasilimali za kibinadamu
  • Biashara ya Ujasiriamali

Bachelor of Arts in Bible and Theology

Bachelor of Arts in Bible and Theology humpa mwanafunzi mafunzo ya nadharia pamoja na mafunzo ya kutumia ujuzi aliyopata kwa ajili ya wito unaohusiana na kanisa. Bachelor of Arts in Counseling

Bachelor of Arts katika Counseling

The Bachelor of Arts in Counseling imekusudiwa kwa wanafunzi ambao wanataka kutumikia kanisa na jamii kwa kutoa huduma za ushauri nasaha kwa watu binafsi, familia ya wanandoa na mahusiano ya jama na Wizara ya ushauri, na vilevile usimamizi wa kundi ndogo na upatanishi.

Master of Arts in Leadership

Hii ni programu ya PAC inayokua kwa kasi zaidi ikiwa na meaneo tatu maluum:

  • Biashara na Ujasiriamali
  • Elimu
  • Wizara za Kikristo

Youth Discipleship Programme

Kwa vijana ambao wamemaliza masomo yao ya shule ya sekondari na wanasubiri elimu ya baada ya sekondari katika vyuo vikuu na taasisi zinginezo.

Intakes[hariri | hariri chanzo]

Intakes za programu za shahada ya kwanza ziko mwezi Septemba na Januari. Intakes za Master of Arts in leadership na youth discipleship ziko Januari tu.

Madarasa ya jioni na Jumamosi[hariri | hariri chanzo]

Kuna madarasa ya jioni katika kampasi ya Nairobi ya PAC huko downtown.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

  • PAC Official Web Site Note: Any text copied from the PAC website is used by permission from the institution