Bonifasia Rodriguez

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha yake halisi.

Bonifasia Rodriguez (jina kamili kwa Kihispaniaː Bonifacia Rodríguez y Castro; Salamanca, Hispania, 3 Juni 1837 - Zamora, Hispania, 8 Agosti 1905) alikuwa sista mwanzilishi mwenza wa shirika la kitawa la Watumishi wa Mt. Yosefu ambalo ndani ya Kanisa Katoliki linahudumia wanawake fukara na wasio na ajira[1].

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 9 Novemba 2003, halafu Papa Benedikto XVI akatangaza mtakatifu tarehe 23 Oktoba 2011[2][3].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

  • Servants of St. Joseph (Kihispania) [1]
  • Vatican News "Bonifacia Rodriguez Castro" [2]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.