Tetemeko la ardhi
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tetemeko la ardhi ni mishtuko ya ghafla ya ardhi. Inatokea mara kwa mara lakini idadi kubwa ni hafifu mno haisikiki na wanadamu ila tu inapimwa na mitambo ya wataalamu.
Yaliyomo |
[hariri] Hatari za mitetemeko ya ardhi
Tetemeko kubwa laweza kusababisha uharibifu mkubwa na vifo hasa kutokana na majengo yanayoanguka. Baharini tetemeko laweza kusababisha tsunami.
[hariri] Sababu
Sababu ya tetemeko ni mara nyingi miendo ya gandunia kama kusukumana kwa mabamba ya ganda la dunia. Katika mazingira ya volkeno tetemeko lasababishwa na miendo ya magma chini ya volkeno hasa wakati wa mlipuko.
Mitetemeko mingi yaani zaidi ya asilimia 80 hutokea katika beseni ya Pasifiki.
[hariri] Vipimo
Wataalamu hupima tetemeko kwa njia mbalimbali. Kuna skeli mbili zinazotumiwa mara nyingi ni zile za Richter na Mercalli.
|
Skeli ya matetemeko ya ardhi kufuatana na Richter na Mercalli |
|||||
|---|---|---|---|---|---|
|
Skeli ya Richter |
Skeli ya Mercalli |
Athira |
Idadi ya mitetemeko ya ardhi |
||
|
Tani TNT |
|||||
|
0 hadi 1.9 |
I |
hupimika kwa mitambo tu, haisikiki na wanadamu |
0.001–0.7 |
(4..4000) |
nyingi sana zaidi ya 700,000 |
|
2 hadi 2.9 |
II |
inasikiwa na watu wachache wakilala pinduli huwa na mwendo kidogo |
1–22 |
(4..90) |
300,000 |
|
3 hadi 3.9 |
III |
husikiwa na watu wachache mishtuko hulingana na lori linalopita bilauri zinazokaa pamoja kabatini zinatoa sauti hafifu |
30–700 |
(0,1..3) |
49,000 |
|
4 hadi 4.9 |
IV hadi V |
hisikiwa na watu wengi. Mwendo wa penduli unaonekana kabisa Bilauri na sahani zatitima, magari huanza kubembea Vitu vinaweza kuanguka |
(1–22) |
(4..90) |
6,200 |
|
5 hadi 5.9 |
VI |
watu hustuka na kukimbia kutoka nyumba zao viti, kabati na vitanda husukumwa kuta za nyumba zapata ufa |
(30–700) |
(0,1..3) |
800 |
|
6 hadi 6.9 |
VII hadi IX |
husikiwa na watu wote wa eneo kwa hofu hata wakiwa kwenye gari nyumba zaanza kubomolewa Miti inabembea kama wakati wa upepo mkubwa Watu hujeruhiwa Kwenye pwani kuna uwezekano wa mawimbi makubwa (chanzo cha tsunami) |
(1–22) |
(4..90) |
120 |
|
7 hadi 7.9 |
X hadi XI |
watu honesha hofu kubwa wakijaribu kutoka nje ya nyumba kwa namna yoyote; nyumba nyingi zaharibiwa ; ufa zatokea katika ardhi; mabomba ya maji na gesi yavunjika watu hujeruhiwa na kuuawa kwenye pwani tsunami inaweza kutokea |
(30–700) |
(0,1..3) |
18 |
|
8 hadi 8.9 |
XII |
uharibifu mkubwa; majengo yote yanaanguka au hayafai tena; maeneo makubwa yaharibiwa Kwenye pwani tsunami hadi kina cha mita 40 |
(1–22) |
(4..90) |
kila baada ya miaka 5 |
|
9.0 na zaidi |
— |
Maafa makubwa; uharibifu kama juu; maisha yote yaweza kuzimwa kimahali Inawezekana pia: vipande vya uso wa ardhi huhamishwa; visiwa kupotea au kutokea; mabamba ya ganda la dunia yaonekana yamesukumwa; |
— |
— |
hakuna tákwimu; tetemeko la aina hili labda kila baada ya miaka 10 hadi 100 |
[hariri] Viungo vya Nje
106