Jengo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jengo kubwa.

Jengo ni tokeo la kudumu la kazi ya binadamu lenye kuta na paa kama vile nyumba, ukumbi au kiwanda. Majengo huwa na kusudi la kutosheleza mahitaji ya watu na jamii kama vile kinga dhidi ya halihewa, mahali pa usalama, mahali pa kuishi na pa faragha, kutunza vitu vyenye thamani, mahali pa kazi.

Majengo huwa na maumbile tofauti sana kutegemeana na vifaa vinavyopatikana, hali ya hewa, gharama za ardhi za kujengea, hali ya ardhi, utamaduni na kusudi linalotarajiwa kwa matumizi ya jengo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: