Historia ya Uholanzi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Historia ya Uholanzi inahusu eneo ambalo siku hizi linaunda Ufalme wa Uholanzi.

Kisha kutekwa na Julius Caesar katika karne ya 1 KK, kusini mwa nchi ikawa mpaka wa kaskazini wa Dola la Roma hadi lilipokoma (karne ya 5).

Baadaye nchi ilivamiwa na makabila mbalimbali ya Wagermanik: Wasaksoni, Wabatavi, Wafrisi na Wafaranki.

Katika karne ya 8 nchi ilikuwa sehemu ya dola la Karolo Mkuu, na katika karne ya 10 ya Dola Takatifu la Kiroma.

Baadaye mfumo wa ukabaila ulitawala nchi sehemu sehemu.

Katika karne ya 16 nchi ilikuwa chini ya familia ya makaisari (Absburg), lakini ilipokea Matengezo ya Kiprotestanti kinyume cha matakwa ya kaisari Karolo V.

Mwanae Filipo II wa Hispania alipomrithi hakukubali jambo hilo na kusababisha uasi ulioenea kote (1566-1581) hadi wilaya saba zilipounda jamhuri iliyotambuliwa na Hispania mwaka 1648 tu, katika amani ya Westfalia.

Karne ya 17 ndipo nchi ilipofikia kilele cha ustawi wake, ikiwa na makoloni mengi huko India, Indonesia, Afrika na Amerika, pamoja na biashara kubwa ya kimataifa duniani kote.

Karne iliyofuata Uingereza ulishika nafasi hiyo ya Uholanzi.

Baada ya mapinduzi ya Kifaransa (1789) nchi ilitekwa na Wafaransa hadi Amani ya Vienna (1814-1815) iliyopanua Uholanzi huru tena, lakini kwa mfumo wa ufalme.

Hata hivyo mwaka 1830 Ubelgiji ulijitenga na mwaka 1890 Luxemburg ilifanya vilevile.

Uholanzi haukutaka kushiriki Vita vikuu vya kwanza vya dunia, lakini katika vita vikuu vya pili ulivamiwa na Ujerumani (1940-1945).

Baadaye Uholanzi umejitahidi sana kushiriki katika mahusiano ya kimataifa na ni kati ya nchi waanzilishi wa Umoja wa Ulaya.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Uholanzi kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.