Desemba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nov - Desemba - Jan
1 2 3 4 5 6 7
8 9 10 11 12 13 14
15 16 17 18 19 20 21
22 23 24 25 26 27 28
29 30 31
Kalenda ya Gregori

Desemba ni mwezi wa kumi na mbili katika kalenda ya Gregori na ni kati ya miezi saba katika kalenda hiyo yenye siku 31.

Tarehe 21 ya mwezi huo wa Desemba (katika miaka mingine inawezekana kuwa tarehe 20 au 22) ni siku ya solistasi ya Kusini (kutoka Kiingereza solstice), yaani wakati Jua linapokuwa kusini kabisa mwa Ikweta.

Neno Desemba limetokana na neno la Kilatini "decem" linalomaanisha "kumi." Desemba ulikuwa ni mwezi wa kumi katika kalenda ya Kirumi.

Simple English Wiktionary
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno: