Yosefu Barsaba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wanafunzi 70 wa Yesu, akiwemo Yosefu Barsaba.

Yosefu Barsaba (pia Yusto, yaani "Mwadilifu") alikuwa mmojawapo kati ya wafuasi wa kwanza wa Yesu.

Kwa msingi huo, baada ya kifo cha Yuda Iskarioti, akawa mmoja kati ya wawili waliopendekezwa kushika nafasi yake kama mtume, lakini bahati ilimuangukia Mathia (Mdo 1:21-26).

Hata hivyo alifanya bidii katika uinjilishaji[1]. Mapokeo ya Kikristo yanasimulia kwamba baadaye akawa askofu wa Eleutheropoli, alipofia dini.

Anaheshimiwa hivyo na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waarmenia kama mfiadini kwa jina la mtakatifu Yusto wa Eleutheropoli. Aliweza kuwa mmojawapo kati ya wakazi wengi waliouawa na Vespasian mwaka 68[2].

Sikukuu yake huadhimishwa nao tarehe 20 Julai[3], 30 Oktoba na 9 Aprili.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/63660
  2. Josephus, Wars of the Jews, Book 4, chapter 8, section 1
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yosefu Barsaba kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.