Wilaya ya Kasese

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Wilaya ya Kasese
Mahali paWilaya ya Kasese
Mahali paWilaya ya Kasese
Mahali pa Wilaya ya Kasese katika Uganda
Majiranukta: 00°11′S 30°05′E / 0.183°S 30.083°E / -0.183; 30.083
Nchi Bendera ya Uganda Uganda
mji mkuu Kasese
Eneo
 - Jumla 2,724 km²
Idadi ya wakazi (2010 Makadirio)
 - Wakazi kwa ujumla 649,400
Tovuti:  http://www.kasese.go.ug

Wilaya ya Kasese ni wilaya iliyoko katika Mkoa wa Magharibi, Uganda. Idadi ya wakazi wake ni takriban 649,400.

Wilaya ya Kasese iko katika ukanda wa ikweta. Inapakana na Wilaya ya Kabarole upande wa kaskazini, Wilaya ya Kamwenge upande wa mashariki, Wilaya ya Rubirizi upande wa kusini, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa magharibi.

Makao makuu ya wilaya yako Kasese, wastani wa km 359 kwa barabara, magharibi mwa Kampala, mji mkuu na mji mkubwa zaidi nchini Uganda.[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Road Distance Between Kampala And Kasese With Map. Globefeed.com. Iliwekwa mnamo 15 April 2014.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]