Usubi-nondo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Usubi-nondo
Usubi-nondo wa bafu (Clogmia albipunctata)
Usubi-nondo wa bafu (Clogmia albipunctata)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Diptera (Wadudu wenye mabawa mawili tu)
Nusuoda: Nematocera (Diptera wenye vipapasio kama nyuzi)
Familia ya juu: Psychodoidea
Familia: Psychodidae
Nusufamilia: Psychodinae
Newman, 1834
Ngazi za chini

Makabilia 6:

Usubi-nondo, visubi-nondo au nzi-nondo (kutoka kwa Kiing. moth flies) ni mbu wadogo wa nusufamilia Psychodinae katika familia Psychodidae ya oda Diptera walio na mabawa makubwa yakilinganishwa na saizi ya mwili na nywele nyingi kama nondo. Spishi fulani, kama Clogmia albipunctata, hujulikana sana, kwa sababu wako kawaida ndani ya mabafu na vyoo za watu ambapo lava wao wanaishi katika mabomba ya kuondoa maji machafu.

Wapevu wa usubi-nondo ni mbu wadogo ambao hawazidi urefu wa mm 5-6. Mwili, miguu na mabawa yao zimefunikwa kwa nywele nyingi ambazo (kwa madume) mara nyingi huwa na rangi na kusababisha ruwaza za rangi. Kwa kawaida macho yao yana umbo la figo na kuwa yameunganishika juu ya kichwa. Kila kimoja cha vipapasio kinajumuisha scape (pingili ya kwanza), pedicel (pingili ya pili) na flagellomere (pingili za mbele) 12-14. Mabawa yana umbo la duaradufu yenye vena 9-10 za mbele hadi nyuma na karibu hakuna vena za kushoto hadi kulia. Spishi za usubi-nondo mara nyingi huonekana sawa na zinatofautishwa tu kwa umbo la sehemu za uzazi za dume.[1]

Mabuu ya usubi-nondo wamegawanyika katika pingili zinazogawanyika na kila mgawanyiko ukiimarishika mgongoni[2]. Mabamba imara za mgongo zina nywele za kweli na za ziada ambazo ni muhimu kwa kutambua spishi[3]. Tofauti na nusufamilia nyingine za Psychodidae fumbatio huishia kwenye neli iliyo na spirakulo kadhaa nchani[2].

Spishi kadhaa za Afrika[hariri | hariri chanzo]

  • Brunettia albonotata
  • Brunettia gloriosa
  • Brunettia obscura
  • Brunettia splendens
  • Clogmia albipunctata
  • Hemimormia nyangerensis
  • Iranotelmatoscopus kenyensis
  • Notoclytocerus carbonarius
  • Notoclytocerus chyuluensis
  • Notoclytocerus fasciatus
  • Potophila verrucosa
  • Psychoda acuta
  • Psychoda albida
  • Psychoda albidonigra
  • Psychoda amphorica
  • Psychoda bilobata
  • Psychoda dentata
  • Psychoda deviata
  • Psychoda dubitata???
  • Psychoda latipennis
  • Psychoda latisternata
  • Psychoda maxima
  • Psychoda modesta
  • Psychoda plumosa
  • Psychoda pseudomaxima
  • Psychoda reducta
  • Psychoda sanfilippoi
  • Psychoda undulata
  • Psychomasina paedagogica
  • Telmatoscopus crassiascoidatus
  • Telmatoscopus edwardsi
  • Telmatoscopus fuscus
  • Telmatoscopus pallidus
  • Telmatoscopus pectinatus
  • Wadicosa benadira
  • Wadicosa cognata

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Wagner, Rüdiger; Koç, Hasan; Özgül, Okan; Tonguç, Alper (2013). "New moth flies (Diptera: Psychodidae: Psychodinae) from Turkey". Zoology in the Middle East (in English) 59 (2): 152–167. ISSN 0939-7140. doi:10.1080/09397140.2013.810880. 
  2. 2.0 2.1 Diptera | What Bug Is That?. Jalada kutoka ya awali juu ya 2022-09-24. Iliwekwa mnamo 2022-09-24.
  3. Kvifte, G. M.; Wagner, R. (2017). "PSYCHODIDAE (Sand Flies, Moth Flies or Owl Flies)". Manual of Afrotropical Diptera. Volume 2. Nematocerous Diptera and lower Brachycera. South African National Biodiversity Institute. ISBN 9781928224129.