Sefania


Nabii Sefania (kwa Kiebrania צְפַנְיָה yaani "Aliyefichwa na Mungu") alikuwa mwana wa Kushi, mtu wa Yerusalemu aliyehubiri kwa nguvu miaka 640-625 hivi KK, yaani mwanzoni mwa utawala wa mfalme Yosia, kabla huyo hajaanza urekebisho wake wa kidini uliofuata kuvumbua hekaluni maandiko ya Kumbukumbu la Sheria.
Ni wakati uleule aliofanya kazi nabii Yeremia, ambaye analingana naye sana.
Habari zake zinatokana tu na kitabu chake ambacho ni cha tisa kati ya vile 12 vya Manabii Wadogo.
Pamoja na kutisha kwa matabiri yake dhidi ya maovu ya watu wa Yuda, yatakayoadhibiwa katika siku ya hasira ya Bwana, alifariji watu maskini na walionewa kwa kuwapa tumaini la wokovu kwamba wao ndio watakaobaki katika Israeli (3:9-20)[1].
Ndio mwanzo wa imani ya kuwa wapenzi wa Mungu ni hasa fukara, ambayo taratibu ilitia mizizi katika Israeli hadi ilipokuja kukaziwa na Yesu (Lk 6:20-21).
Tangu kale Sefania anaheshimiwa kama mtakatifu.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sefania kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |