Mlima wa Mizeituni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mlima wa mizeituni mnamo Julai 2009.

Mlima wa Mizeituni ni mlima unaopatikana mashariki mwa jiji la kale la Yerusalemu.

Mlima huu ulipewa jina la Mizeituni kwa sababu ya miti ya mizeituni ambayo inauzunguka mlima huo. Sehemu ya kusini ya Mlima huu ilikuwa necropolis ya Silwan, inayohusishwa na ufalme wa kale wa Uyahudi. Mlima huu unatumika kama makaburi ya Wayahudi kwa zaidi ya miaka 3,000 na huchukua takriban makaburi 150,000, na kuufanya kuwa kati ya utamaduni wa makaburi ya Kiyahudi.

Matukio kadhaa muhimu katika maisha ya Yesu, kama yanavyosimuliwa katika Injili, yalifanyika kwenye Mlima wa mizeituni, na katika Matendo ya Mitume inaelezewa kama mahali ambapo Yesu alipaa kwenda mbinguni. Kwa sababu ya uhusiano wake na Yesu na Bikira Maria, mlima huu umekuwa sehemu ya ibada ya Kikristo tangu nyakati za zamani; hata leo ni sehemu kuu ya hija kwa Wakatoliki.

Sehemu kubwa ya kilele cha Mlima wa Mizeituni hukaliwa na At-Tur, kijiji cha zamani ambacho sasa ni kitongoji cha Mashariki mwa Yerusalemu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]