Mzeituni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mzeituni
(Olea europaea)
Mzeituni
Mzeituni
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Planta (mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Asterids (Mimea kama alizeti)
Oda: Lamiales (Mimea kama guguchawi)
Familia: Oleaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mzeituni)
Jenasi: Olea
Spishi: O. europaea
L.

Mzeituni au mzaituni (jina la kisayansi kwa Kilatini Olea europaea, yaani "mzeituni wa Ulaya", au Olea sylvestris, yaani "mzeituni mwitu") ni mti mfupi wa familia ya Oleaceae unaopatikana hasa kandokando ya Bahari ya Kati, lakini pia sehemu nyingine za Afrika na Asia.[1]

Matunda yake (zeituni au zaituni) ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa mafuta (90%), ingawa yanaliwa pia bila kushindiliwa (10%).

Inaonekana asili ya ulimaji wake ni Uajemi na Mesopotamia miaka 6,000-7,000 iliyopita. Kutoka huko ulienezwa sehemu nyingine.

Leo uzalishaji ni mkubwa hasa Hispania, halafu Italia, Ugiriki, Uturuki n.k.

Mbali ya faida hiyo, toka zamani tawi la mti huo linatazamwa kama ishara ya wingi, utukufu na amani. Kwa sababu hiyo lilitolewa kwa miungu na kwa washindi.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Simple English Wiktionary
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno:
Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mzeituni kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.