Nenda kwa yaliyomo

Majadiliano ya mtumiaji:Abubakari Sixberth

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Weka mada
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Latest comment: miezi 2 iliyopita by Abubakari Sixberth in topic Vigezo na kwa Lugha ya Kiswahili

Karibu kwenye Wikipedia kwa Kiswahili!

Tunamfurahia kila mmoja anayeingia na kuungana nasi. Hii ni kamusi elezo ya maandishi huru. Unaweza kuandika makala uipendayo ama kuitafsiri kutoka Wikipedia ya lugha nyingine.

Ukipenda kutumia kurasa zetu za mwongozo na msaada, a) ukitumia simu bofya kwa "Dawati" chini kwenye dirisha lako na b) ubadilishe mwonekano wa Wikipedia kwa kubofya "Switch to old look" kwenye menyu upande wa kushoto.

Kwa mawili matatu labda tazama:

Jisikie huru kuuliza swali lolote lihusianalo na Wikipedia hii. Karibu kujitambulisha kwenye "Ukurasa wa mtumiaji". Ukitaka kupata kwanza uzoefu wa kuweza kuhariri Wikipedia, tafadhali tumia ukurasa wako kwa majaribio. Humo unaruhusiwa kujipatia uzoefu wa uundaji wa makala za Wikipedia! Juu yako mwenyewe uandike tu kwenye ukurasa wako wa mtumiaji. Humo uko huru kutangaza chochote upendacho, kama si biashara au matusi.

Ujue miiko:

  • usilete kamwe matini wala picha kutoka tovuti za nje.
  • usiingize matangazo ya kibiashara (pamoja na kuelekeza kwa kurasa zenye matangazo).
  • usimwage kamwe matini kutoka google-translate au programu za kutafsiri.
  • usitumie kama vyanzo vya taarifa au tanbihi <ref>Wikipedia (au mradi mwingine wa Wikimedia)</ref>, ila unaweza kutumia vyanzo vyake kwa kuvitaja vyenyewe moja kwa moja.

Tunakushauri pia kuandikisha email yako; haitaonekana na wengine lakini wataweza kukuandikia kupitia mfumo wa Wikipedia. Karibu sana!


Welcome to Kiswahili Wikipedia!

We welcome you even if you don't speak Kiswahili. For a bot flag go to this site. If you try to edit entries as a non-speaker, it is better to first communicate with one of our admins who can advise you. You may find them at Wikipedia:Wakabidhi. And, please:

  • do not post computer translated texts (like Google Translate, Content Translation, etc. all do not work for Swahili)
  • nor copied texts/images from other webs to this site!
  • do not use links to commercial pages, never post anything that looks like advertising.
  • do not use as references <ref>Wikipedia (or another project of Wikimedia)</ref>, though you can use their references by writing them themselves.

As a newcomer we advise that you register your email. This will not be visible to others but it allows us to notify you, which often is helpful in case of problems.

Idd ninga (majadiliano) 22:03, 23 Aprili 2022 (UTC)Reply

Google Translate

[hariri chanzo]

Asante kwa michango yako, lakini napaswa kudokeza tatizo. Katika makala ulizoanzisha kuhusu Wilson Kinyonga na George Konyonga nimeona dalili kwamba ulitumia Google Translate bila kusafisha vizuri. Mfano: uliandika "Nyota bora wa Wanyika" kama tafsiri ya Wanyika Super Stars; ambayo kwa Kiswahili haina maana kabisa, tena ni kosa kwa sababu majina hayatafsiriwi. Naomba sana uwe mwangilifu, maana wachangiaji wanaomwaga matini kutoka tafsiri ya komyuta wanazuliwa hapa. Kipala (majadiliano) 10:30, 1 Mei 2022 (UTC)Reply

Vizuri kusikia kutoka kwako 217.29.135.51 08:29, 2 Mei 2022 (UTC)Reply

Interwiki

[hariri chanzo]

Tafadhali urudi kwenye makala zako ulizotafsiri juzi na uongeze interwiki. Kipala (majadiliano) 10:42, 22 Mei 2023 (UTC)Reply

Taarifa ya kukuzuia!

Ndugu, imenibidi kukuzuia kwa sababu zinazotajwa chini. Wakati unapokuwa umezuiwa huwezi kuhariri isipokuwa penye huu ukurasa wako wa majadiliano. Unaweza kunijibu kwa kutumia “Email this user”.

Sababu ni kuwa umeingiza matini iliyopatikana kwa njia ya tafsiri ya kompyuta ikiwa na kasoro nzito ya lugha. Umearifiwa kwamba ni marufuku kumwaga matokeo ya google translate katika makala zetu. Wachangiaji wanaopuuza utaratibu huu wanasababisha hasara kubwa kwa Wikipedia yetu na kuwapa wengine kazi kubwa mno ya kusafisha makosa yao.

Bila shaka una nia nzuri kuchangia katika Wikipedia. Tutafurahi kushirikiana nawe lakini ni lazima ufuate utaratibu. Kazi yetu kama wakabidhi ni kulinda mradi huu.

Ukiwa tayari kufuata utaratibu pamoja na kupitia upya matini ulizozileta tayari, naomba uwasiliane nami kwa kufungua ukurasa wangu (bofya jina langu chini) na kuniandikia baruapepe kwa kubofya “Email this user” upande wa kushoto. Hapo nitaweza kukuruhusu tena. Hapo lazima uwezeshe njia kwa kufuata maelezo katika Wikipedia:Email.

Nimeona umetumia tafsiri ya kompyuta bila masahihisho ya kutosha; mifano Faiza Darkhani, Nina Amenta, Malawi Girl Guides Association. Kipala (majadiliano) 20:12, 22 Mei 2023 (UTC)Reply

Marekebisho ya Makala ya Faiza Darkhani.

[hariri chanzo]

Faiza Darkhani (alizaliwa 1992) ni mwalimu, mwanamazingira na mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Afghanistan.[1] Mnamo mwaka 2021, alitajwa katika orodha ya wanawake 100 wa BBC inayojumuisha majina ya wanawake wenye msukumo na ushawishi mkubwa duniani.[2] Darkhani ni miongoni mwa wasomi wachache waliopata elimu ya sayansi ya tabianchi huko Afghanistan.[2] Pia alikuwa mkurugenzi kwenye Shirika la taifa la Kulinda Mazingira katika jimbo la Badakhshan, Afghanistan.[1]

Alisoma chuo kikuu cha Badakhshan pamoja na chuo kikuu cha Putra Malaysia na kupata shahada ya uzamili ya sanyansi katika usanifu wa mazingira.[1] Utafiti wake unahusisha usimamizi endelevu wa mandhari mijini pamoja na usalama wa chakula.[3]

Marejeo

  1. 1 2 3 "BBC 100 Women 2021: Who is on the list this year?". BBC News (kwa Kiingereza (Uingereza)). 2021-12-07. Iliwekwa mnamo 2022-04-23.
  2. 1 2 "50 Afghans among BBC's 100 influential women of 2021". The Frontier Post (kwa American English). 2021-12-08. Iliwekwa mnamo 2022-04-24.
  3. Bohn, Katrin; Viljoen, André. "The vision of productive urban landscapes is horizontal and vertical". Productive Urban Landscapes. University of Brighton, UK. Iliwekwa mnamo 2022-04-23.

Abubakari Sixberth (majadiliano) 08:57, 11 Juni 2023 (UTC)Reply

Editathon

[hariri chanzo]

Ndugu, inaonekana umehusika na mpango wa Editathons wiki iliyopita. Kwa kweli imeharibu sana. Msifanye tena hivyo. Mjiandae zaidi na kutushirikisha sisi wakabidhi, tafadhali. Amani kwako!--Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:51, 25 Desemba 2024 (UTC)Reply

Ahsante kwa kuniandikia katika ukurasa wangu. Nimefurahi kusikia kutoka kwako, hata hivyo tunapitia kila rekebisho lililofanywa na wahariri ili kuangalia makosa waliyofanya katika kila hariri. Ahsante na Amani iwe juu yako. Abubakari Sixberth (majadiliano) 17:28, 25 Desemba 2024 (UTC)Reply

NO such thing as their editing correction ever occurred. Thus both special:contribs/~2024-30796 and I already cleared the mess. Resnick-mike (majadiliano) 17:40, 25 Desemba 2024 (UTC)Reply

Vigezo na kwa Lugha ya Kiswahili

[hariri chanzo]

Ndugu, epuka kuweka matini ya lugha isiyo kiswahili kwenye Wiki ya Kiswahili, mfano vigezo, matukio na majina ya makala. Nimetafsiri vigezo ulivyoweka. Wiki ya kiswahili ni mahususi kwa kiswahili, fikiria kwamba kuna mtu atahitaji kunufaika na matini na makala uliyoweka ambaye hana ujuzi na lugha nyingine tofauti na kiswahili. Amani kwako. Czeus25 Masele (majadiliano) 06:36, 24 Oktoba 2025 (UTC)Reply

Habari ndugu, Czeus25 Masele, Asante kwa kuniandikia katika ukurasa wangu wa majadiliano. Ninapenda kukujuza kwamba tunaendelea na mafunzo kutoka Wikimedia Foundation na kuhusu vigezo, warsha pamoja majina ya kampeni kuwa katika lugha ya kiingireza imetokana na kutengenezwa kufuatia majina ya kampeni tunazoziendesha. Hivyo basi, tunaomba urejeshe majina yaliyobadiliswa kuwa kama awali. Ahsante na Amani kwako. Abubakari Sixberth (majadiliano) 07:27, 24 Oktoba 2025 (UTC)Reply
Kwa kweli mimi pia nashangaa kuona matukio ya Wikipedia ya Kiswahili kuwa yote ya Kiingereza! Tunataka kueleweka au kujipendekeza kwa nani? Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:03, 28 Novemba 2025 (UTC)Reply
Habari za wakati huu Mheshimiwa, Riccardo Riccioni, Nashukuru kwa kuniandia katika ukurasa wa Majadiliano. Ningependa kuelezea jambo kwamba hatuna maana ya kuharibu miiko yetu ya Wikipedia ya Kiswahili bali matukio haya yameandikwa kwa kingereza kwa sababu tupo kwenye mafunzo kutoka Wikimedia Foundation. Baada ya mafunzo kuisha, matukio haya yatahaririwa kwa lugha ya kiswahili. Ahsante na Amani kwako. Abubakari Sixberth (majadiliano) 15:01, 28 Novemba 2025 (UTC)Reply
Unaendelea kutunga kurasa kwa lugha ya Kiingereza kuhusu matukio mliyoyaandaa. Si sawa kabisa. Hii ni Wikipedia ya Kiswahili!!! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:17, 6 Desemba 2025 (UTC)Reply
Tunaanza kuyafanyia kazi matukio yote ya nyuma kuyarejesha kwa lugha yetu adhimu ya kiswahili. Niwie radhi, ila kwa wakati huu tunalazimika kuyatengeneza kwa lugha ya kiingereza kwa kuwa mkufunzi wetu anayetuelekeza namna sahihi ya kuaandaa matukie kulingana na programu zetu za mwaka hafahamu lugha ya kiswahili hata kidogo. Ila naomba nikuhakikishie kwamba maelezo ya matukio haya yote tutayaweka kwa lugha yetu. Ahsante tena na tena kwa kunikumbusha wajibu wangu. Abubakari Sixberth (majadiliano) 19:00, 10 Desemba 2025 (UTC)Reply
Yaleyale. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 05:19, 22 Machi 2026 (UTC)Reply
Ahsante kwa kutukumbusha tena. Tukio hili pia lilitengenezwa wakati ule wa mafunzo. Na wenyewe tutaurejesha kwa kiswahili punde tu shindano litakapo isha kama tulivyofanya kwa zile zilizopita. Pia nilikua ninaombi la kurejeshwa kwa lile tukio lingine lililofutwa maana na lenyewe litafanyiwa kazi. Amani kwako. Abubakari Sixberth (majadiliano) 08:01, 22 Machi 2026 (UTC)Reply

Jamii

[hariri chanzo]

Ndugu, hongera kwa umakini wako katika kusahihisha makala nyingi. Naomba uongeze jamii chini. Kwa mfano, [[Jamii:Wachezaji mpira wa Guinea]] baada ya zile zilizopo tayari. Amani kwako!--Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:49, 14 Machi 2026 (UTC)Reply