Magofu ya Tongoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Magofu ya Tongoni Wilayani Tanga.

Magofu ya Tongoni ni magofu ya Waswahili yaliyorekodiwa karne ya 15. Magofu hayo ya msikiti na makaburi arobaini yako katika kata ya Tongoni, Wilaya ya Tanga, iliyomo ndani ya Mkoa wa Tanga, nchini Tanzania.

Kinyume na uwepo wake ambao hauonekani leo, Tongoni ulikuwa mji na kitovu cha biashara cha Waswahili kilichostawi na kuheshimiwa sana katika karne ya 15. Mengi ya magofu ya Tongoni bado hayajafichuliwa. [1]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mji mkongwe wa Tongoni ulianzishwa na Waswahili karibu na karne ya 11 kama sehemu ya majimbo ya miji mbalimbali ya Uswahilini iliyo kando ya pwani ya Afrika Mashariki. [2] [3]

Vasco da Gama, baharia wa Ureno, alitembelea mji wa Tongoni kwa mara ya kwanza mnamo mwezi wa Aprili 1498. Alipata fursa ya kula machungwa ya kienyeji kwenye mji huo, ambayo alisema ni bora kuliko yale yanayopatikana kwao Ureno. Alifanya ziara ya pili mwaka uliofuata, 1499 na alikaa siku kumi na tano mjini Tongoni. [4]

Usimamizi[hariri | hariri chanzo]

Magofu ya mji wa kale wa Tongoni yako chini ya Idara ya Mambo ya Kale ya Tanzania kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii. Magofu yako wazi kwa umma, lakini hakujawa na uchimbaji wa awamu ya tatu. Kati ya miongo kadhaa iliyopita, uchunguzi kiasi wa majaribio ulifanyika na mpango wa eneo ulichorwa, lakini bado uchimbaji haujaanza. [5]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Mabulla, Audax Z. P. “Strategy for Cultural Heritage Management (CHM) in Africa: A Case Study.” The African Archaeological Review, vol. 17, no. 4, Springer, 2000, pp. 211–33, http://www.jstor.org/stable/25130707.
  2. Lane, Paul J. “Maritime and Shipwreck Archaeology in the Western Indian Ocean and Southern Red Sea: An Overview of Past and Current Research.” Journal of Maritime Archaeology, vol. 7, no. 1, Springer, 2012, pp. 9–41, http://www.jstor.org/stable/43551368.
  3. Askew, Kelly M. “Female Circles and Male Lines: Gender Dynamics along the Swahili Coast.” Africa Today, vol. 46, no. 3/4, Indiana University Press, 1999, pp. 67–102, http://www.jstor.org/stable/4187285.
  4. Lane, Paul J. “Maritime and Shipwreck Archaeology in the Western Indian Ocean and Southern Red Sea: An Overview of Past and Current Research.” Journal of Maritime Archaeology, vol. 7, no. 1, Springer, 2012, pp. 9–41, http://www.jstor.org/stable/43551368.
  5. https://www.maliasili.go.tz/uploads/Mafanikio_ktk_Idara_ya_Mambo_ya_Kale.pdf