Lamadi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Lamadi ni mji mdogo na kata ya Wilaya ya Busega katika Mkoa wa Simiyu, Tanzania, yenye postikodi namba 39507 [1].

Mitaa yake ni Itongo, Makanisani, Majengo, Msekula Road, Mwalukonge, Kisesa na vijiji vitatu ambavyo ni Lukungu, Mwabayanda na Kalago (Mwabulugu Lakeshore).

Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2022, kata ilikuwa na wakazi wapatao 44,146 waishio humo.[2]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 22,062 waishio humo.[3].

Wakazi walio wengi ni wa makabila ya Wasukuma, Wajita, Wakurya, Wazanaki na Waha.

Mji wa Lamadi umepakana na Ziwa Viktoria upande wa Magharibi, Pori la Akiba Kijereshi na Kata za Lutubiga na Mkula upande wa Mashariki, Wilaya ya Bunda upande wa Kaskazini na Kata ya Kalemela upande wa Kusini. Mji wa Lamadi ufikika kwa Barabara za kitaifa ambazo ni Barabara ya Mwanza to Musoma, pamoja na Barabara ya Shinyanga,Bariadi to Lamadi.

Mji wa Lamadi ni maarufu kwa biashara, uvuvi, utalii, kilimo na ufugaji.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Busega - Mkoa wa Simiyu - Tanzania

Badugu | Igalukilo | Imalamate | Kabita | Kalemela | Kiloleli | Lamadi | Lutubiga | Malili | Mkula | Mwamanyili | Ngasamo | Nyaluhande | Nyashimo | Shigala

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Simiyu bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.