Lambo la Kihansi

Majiranukta: 08°34′30.0″S 35°51′05.0″E / 8.575000°S 35.851389°E / -8.575000; 35.851389
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kihansi)

08°34′30.0″S 35°51′05.0″E / 8.575000°S 35.851389°E / -8.575000; 35.851389


Lambo la Kihansi linapatikana nchini Tanzania katika mkoa wa Morogoro na linaunda bwawa la maji ya mto Kilombero litumikalo kuzalisha umeme kwa njia ya kani mvutano yaani graviti.

Bwawa la Kihansi lina uwezo wa kuzalisha hadi megawatts 180 (241,384 hp) ambapo linachangia asilimia 13 ya umeme unaozalishwa nchini Tanzania [1].

Mahali[hariri | hariri chanzo]

Bwawa la Kihansi, ambalo limetokana na lambo hilo, linapatikana kusini mwa Tanzania kukatisha mto Kilombero katika korongo la Kihansi baada ya kukutana na mto ulanga. Kutoka Dar es Salaam inakadiriwa kuwa kilometa 643 kusini[2], wakati kutoka Iringa inakadiriwa ni kilometa 168 kusini, mpakani mwa Wilaya ya Mufindi na Wilaya ya Kilombero[3].

Historia[hariri | hariri chanzo]

Bwawa la Kihansi linamilikiwa na shirika la umeme la Tanzania TANESCO. Lilianza kujengwa mnamo Julai 1995 likakamilika na kisha kufunguliwa na Rais wa awamu ya tatu wa Tanzania, Benjamin W. Mkapa tarehe 10 Julai 2000.

Ujenzi wake uligharimu kiasi cha dola za Kimarekani milioni 275 [1][4].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 Power Technology (2020). "Lower Kihansi Hydropower Project". London: Power-Technology.com. Iliwekwa mnamo 1 August 2020.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. https://www.google.com/maps/dir/Dar+es+Salaam,+Tanzania/Kihansi+hydro+power+plant,+Mlimba,+Tanzania/@-7.4264117,35.1951065,7z/data=!3m1!4b1!4m14!4m13!1m5!1m1!1s0x185c4bae169bd6f1:0x940f6b26a086a1dd!2m2!1d39.2083284!2d-6.792354!1m5!1m1!1s0x18ff51e3aa0196e1:0x390dbda175a80b24!2m2!1d35.8089055!2d-8.7824511!3e0
  3. https://www.google.com/maps/dir/Iringa,+Tanzania/Mlimba,+Tanzania/@-8.2750734,35.0682795,9z/data=!3m1!4b1!4m14!4m13!1m5!1m1!1s0x1854162bc11b2eb1:0x287d3378c421502f!2m2!1d35.6860723!2d-7.768059!1m5!1m1!1s0x18ff51ea3e353cd7:0x2e4e348437939e6e!2m2!1d35.8089055!2d-8.7824511!3e0 |access-date=1 August 2020
  4. Pierre Julien and Seema Shah (1 November 2005). "Sedimentation Initiatives in Developing Countries" (Archived from the original on 26 July 2011). UNESCO. ku. 29–31. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 26 July 2011. Iliwekwa mnamo 16 May 2010.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); More than one of |archiveurl= na |archive-url= specified (help); More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help); More than one of |archivedate= na |archive-date= specified (help); Check date values in: |date=, |archivedate=, |accessdate= (help)

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Iringa bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Lambo la Kihansi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.