Kaniko abati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake huko Kilkenny.

Kaniko abati (pia: Cainnech, Kenneth au Kenny; Kinnaght, 525 hivi  – Ossory, 600 hivi) alikuwa mmonaki padri kutoka Ireland, maarufu kwa kuanzisha monasteri nyingi na kueneza Ukristo wa Kiselti katika sehemu mbalimbali za visiwa vya Britania, akifanya umisionari[1] pamoja na kushika kanuni kali ya kitawa[2][3].

Aliandika kitabu cha ufafanuzi wa Injili[4].

Anahesabiwa kati ya Mitume kumi na wawili wa Ireland.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 11 Oktoba[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.