Jeanne d'Arc

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jeanne d'Arc

Jeanne d'Arc (mnamo 1412Rouen, 30 Mei 1431) alikuwa msichana Mfaransa anayeheshimiwa kama shujaa wa uhuru wa Ufaransa na mtakatifu wa Kanisa Katoliki.

Tarehe 18 Aprili 1909 alitangazwa na Papa Pius X kuwa mwenye heri na tarehe 16 Mei 1920 Papa Benedikto XV alimtangaza mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyouawa.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Aliongoza jeshi la Ufaransa katika kipindi kimoja cha Vita vya Miaka 100 dhidi ya Uingereza akawashinda Waingereza na kuhakikisha uhuru na umoja wa Ufaransa.

Baadaye alikamatwa na Waingereza akahukumiwa kuchomwa moto na mahakama ya Wafaransa walioshirikiana na Waingereza kwa tuhuma za kuwa mzushi na mwasi wa Mungu zisizokuwa na msingi wowote.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.