Historia ya awali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Göbekli Tepe, leo kusini-mashariki mwa nchi ya Uturuki, ilijengwa miaka 11,000 hivi iliyopita. Haya ndiyo mabaki yake.

Historia ya awali (kwa Kiingereza: prehistory) ni kipindi kirefu sana cha historia, kikichukua miaka yote tangu binadamu walipotokea duniani mpaka historia andishi ilipoanza (huko Mesopotamia miaka 3,300 hivi KK).[1]

Ingawa muda ni mrefu sana na ni wa msingi kwa historia yote iliyofuata, watu hawakuwa wengi kama walivyozidi kuwa kadiri ya maendeleo yao. Maisha yao hayakuwa marefu kutokana na ugumu wa mazingira na utovu wa vifaa na dawa mbalimbali.

Jina[hariri | hariri chanzo]

Katika lugha nyingi msamiati ni kabla ya historia (k.mf. kwa Kiingereza ni pre-history), ambao unatokana na maneno ya Kigiriki προ, pro, yaani "kabla" na ιστορία, istoria, yaani "historia").

Paul Tournal mwanzoni alitunga neno la Kifaransa “Pré-historique” katika kuelezea ugunduzi aliofanya katika mapango ya kusini mwa Ufaransa.

Neno hilo lilitumika katika Ufaransa kuanzia miaka ya 1830 kuelezea kipindi kabla ya uandishi, na baadaye likaingizwa na Daniel Wilson katika Kiingereza mwaka 1851.

Vipindi vya historia ya awali[hariri | hariri chanzo]

Sehemu kubwa kabisa ya historia ya binadamu ilitokea kabla ya maandishi kugunduliwa. Kuhusu zamani hizo tunapata habari kutokana na utafiti wa akiolojia.

Kwa njia hiyo tunakuta mabaki ya ya siku zile kama vile vifaa, majengo au pia uchoraji kwenye kuta za mapango lakini tunakosa maelezo jinsi yanavyopatikana tangu watu waanze kuandika kumbukumbu.

Kati ya vipindi vya historia ya awali ni zama za mawe. Wakati huo wote watu walipiga hatua muhimu ya maendeleo, kama vile kubuni vifaa vya kwanza, kilimo, na kujenga vijiji na miji ya kwanza.

Hata vyanzo vya teknolojia za metali, kama zama za shaba na zama za chuma, vilitokea kabla ya kugundua maandishi katika sehemu nyingi za dunia.

Lakini mifano ya kwanza ya utamaduni wa kimaandishi ilitokea wakati wa kubuni matumizi ya shaba na bronzi huko Misri na Mesopotamia.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Shotwell, James Thomson. An Introduction to the History of History. Records of civilization, sources and studies. New York: Columbia University Press, 1922.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya awali kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.