Nenda kwa yaliyomo

Goeriki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Goeriki katika mavazi ya ibada ya kiaskofu.

Goeriki (pia: Goheric, Goderic, Goëry, Goeric, Goericus, Goéry, Abbo, Appo, Abdo, Albo; Albi, leo nchini Ufaransa[1], 565/575 [2] - 643 hivi) alikuwa mwanajeshi mwenye cheo kikubwa[3] chini ya Dagobati I, mfalme wa Austrasia.

Baba wa mabinti wawili, ambaye mmojawao (Prisia) anaheshimiwa kama mtakatifu bikira, mwaka 627 alichaguliwa kuwa askofu wa Metz[4] baada ya Arnulfo, ambaye labda alikuwa jamaa yake na alimpa upadirisho, kwenda kwa siri kuishi kama mkaapweke karibu na monasteri ya Hamend iliyoanzishwa na rafiki yake Amato[5].

Arnulfo alipofariki, Goeriki alihamisha kwa heshima zote masalia yake mjini Metz [6].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Septemba[7].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. (Kiingereza)Archdiocese of Albi (Albia). Goyau, G. (1907) In The Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company
  2. (Kiingereza) Butler's Lives of the Saints p. 182 Alban Butler, Paul Burns 1995 ISBN 0-86012-258-1
  3. Saint Goëric Archived 2008-06-19 at the Wayback Machine Daniel Bigerel, Cercle d'études locales de Houdemont
  4. Michael Walsh, mhr. (2001). Dictionary of Christian Biography. Continuum. uk. 2. ISBN 0826452639.
  5. http://www.santiebeati.it/dettaglio/63350
  6. https://www.santiebeati.it/dettaglio/70790
  7. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • (Kiingereza) Frederick G. Holweck, A Biographical Dictionary of the Saints. St. Louis, MO: B. Herder Book Co., 1924.
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.