Siri

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pengine siri ni suala la uhai au kifo, kama wakati wa Vita vikuu vya pili.

Siri (kutoka neno la Kiarabu) ni jambo lolote ambalo mtu analiona haifai kumshirikisha mtu yeyote yule, haijalishi ni nani.

Kila mmoja ana haki ya kuwa na siri zake.

Katika maisha ya jamii, siri ni muhimu, kiasi kwamba ni wajibu kwa baadhi ya kazi, kama vile ushauri, uganga, huduma za benki n.k.

Siri kali zaidi, katika Kanisa Katoliki, ni ile ya padri kuhusu maungamo aliyopokea katika sakramenti ya kitubio.