Filogoni wa Antiokia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Filogoni wa Antiokia (alifariki Antiokia, leo nchini Uturuki, 324) alikuwa askofu mkuu wa mji huo kuanzia mwaka 314 hadi kifo chake[1] .

Kwanza alioa na kuzaa binti; alikuwa wakili maarufu kwa kutenda haki.

Baadaye alishika uongozi wa jimbo na kupinga Uario.

Hatimaye alifungwa kwa ajili ya imani katika dhuluma ya kaisari Licinius.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 20 Desemba[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.