Erling Braut Håland

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
haaland akicheza dhidi ya wolfsburg
Haland akiwa na mpira.
Haaland alipokua kwenye mechi ya Ligi ya raundi ya pili ya Bundesliga ya Austria

Erling Braut Haaland (alizaliwa 21 Julai 2000) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Norway ambaye anacheza kama mshambuliaji wa klabu ya Uingereza Manchester City kwenye Mashindano ya Ligi kuu ya Uingereza na timu ya taifa ya Norway.

Anachukuliwa kuwa ni mmoja wa wachezaji bora zaidi ulimwenguni, anajulikana kwa uchezaji wake, kasi na umaliziaji.[1]

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Haaland alizaliwa mnamo 21 Julai 2000 huko Leeds, Uingereza, kwani baba yake Alfie Haaland alikuwa akiichezea klabu ya Leeds United kwenye Ligi ya Klabu bingwa barani Ulaya wakati huo.[2] Mnamo 2004, akiwa na umri wa miaka mitatu, alihamia Bryne, mji ambapo wazazi wake wanaishi huko Norwei.[3][4]

Pamoja na kucheza kandanda tangu utotoni, Haaland alishiriki katika michezo mingine mbali mbali pindi alikua mtoto, ikiwa ni pamoja na mpira wa mikono,gofu na riadha.[5] Pia inasemekana alipata rekodi ya dunia katika kitengo cha umri wake kwa kuruka kwa umbali mrefu alipokuwa na umri wa miaka mitano, na umbali uliorekodiwa ni mita 1.63 mnamo mwaka 2006.[6]

Håland alianza kazi yake katika klabu ya nyumbani kwake Bryne FK mnamo 2016, na alihamia Molde FK mwaka uliofuata ambapo alitumia miaka miwili. Mnamo Januari 2019 alihamia upande wa Austria Red Bull Salzburg kwa mkataba wa miaka mitano. Alicheza katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya (UEFA) ya 2019-20, alikuwa kijana mdogo kuliko wote kucheza mechi tano mfululizo za Ligi ya Mabingwa ya UEFA.

Mnamo 29 Desemba 2019, Håland alihamia Borussia Dortmund ya Ujerumani kwa ada iliyoripotiwa kuwa milioni 20.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Is Erling Haaland the best striker in the world?. Optus Sport (25 November 2020).
  2. Cross, Beren. "Wonderkid Haaland would pick Leeds United over Man Utd every time", 9 July 2018. "Erling Braut Haaland was born in Leeds in July 2000, a short time after his father, Alf-Inge, departed Elland Road for Manchester City after three years in West Yorkshire." 
  3. Hansen, Ole Jonny Eriksrud (29 November 2018). Erling Braut Haaland: – Har sagt til meg selv at jeg vil bli verdens beste spiller (no).
  4. Rose, Gary. "Erling Braut Haaland: Is Red Bull Salzburg striker really 'the next Zlatan Ibrahimovic'?", 2 October 2019. 
  5. "Erling Haaland: "I clicked with Jadon Sancho, Marco Reus and Thorgan Hazard straight away"", 14 February 2020. 
  6. Arora, Mudeet (19 February 2020). Stunning Report Reveals Erling Braut Haaland is a World Record Holder in Athletics. Jalada kutoka ya awali juu ya 2021-04-16. Iliwekwa mnamo 2022-11-29.
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Erling Braut Håland kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.