Nenda kwa yaliyomo

Diego wa Alkala

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Diego akiwa ametoka nje ya nafsi yake mbele ya msalaba, mchoro wa Murillo, 1645-6.
Mtakatifu Diego

Diego wa Alkala, O.F.M. (San Nicolás del Puerto, Sevilia, Hispania, 1400 hivi - Alcalá de Henares, Hispania, 12 Novemba 1463) alikuwa bruda wa shirika la Ndugu Wadogo aliyeng'aa kwa upendo kwa wagonjwa[1].

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu. Alitangazwa kuwa hivyo na Papa Sixtus V mwaka 1588.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Novemba[2].

Alifanya kazi ya umisionari katika visiwa vya Kanaria (karibu na pwani ya Moroko).

Alipohiji Roma kwa Jubilei alijitosa kuhudumia waliopatwa na tauni.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Marejeo ya Kiswahili

[hariri | hariri chanzo]
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 403-404
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 556-557

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.