Buhangaza

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Buhangaza ni kata ya Wilaya ya Muleba katika Mkoa wa Kagera, Tanzania, yenye postikodi namba 35538 [1].

Kijiografia imezungukwa na mto maarufu kwa jina la mto Ngono na milima ya ikunjo.

Kata hiyo inaundwa na vijiji vinne ambavyo ni: Buyaga, Buhangaza, Kashenge na Rwenshato.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 6,350 [2].Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 6,603 waishio humo.[3]

Kata hii ina jumla ya shule tatu za msingi ambazo ni pamoja na Buhangaza, Rwenshato na Buyaga, pia ina shule moja ya sekondari ya Ikondo.

Katika kata hii shughuli kuu za kiuchumi ni pamoja na kilimo cha zao la kahawa pamoja na migomba. Shughuli nyingine ndogondogo zinazofanyika katika kata hii pamoja na kilimo, ni biashara, uvuvi na ufugaji.

Chakula cha asili, kama ilivyo kwa mkoa wote wa Kagera, ni ndizi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2018-08-05. Iliwekwa mnamo 2018-02-01. 
  2. https://www.nbs.go.tz, uk 172
  3. Sensa ya 2012, Kagera - Muleba-District-Council
Kata za Wilaya ya Muleba - Mkoa wa Kagera - Tanzania

Biirabo | Bisheke | Buganguzi | Buhangaza | Bulyakashaju | Bumbire | Bureza | Burungura | Goziba | Gwanseli | Ibuga | Ijumbi | Ikondo | Ikuza | Izigo | Kabirizi | Kagoma | Kamachumu | Karambi | Kasharunga | Kashasha | Katoke | Kerebe | Kibanga | Kikuku | Kimwani | Kishanda | Kyebitembe | Mafumbo | Magata Karutanga | Mayondwe | Mazinga | Mubunda | Muhutwe | Muleba | Mushabago | Ngenge | Nshamba | Nyakabango | Nyakatanga | Ruhanga | Rulanda | Rutoro


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Buhangaza kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.