Wilaya ya Muleba

Wilaya ya Muleba ni wilaya mojawapo kati ya 8 za Mkoa wa Kagera, Tanzania yenye postikodi namba 35500 [1]. Makao makuu yako kwenye mji wa Muleba.
Muleba ilikuwa tarafa ya Bukoba ikaanzishwa kama wilaya ya pekee mwaka 1984. Kwa sasa ina tarafa tano: Muleba, Kimwani, Nshamba, Izigo na Kamachumu. Eneo la wilaya ni kilomita za mraba 3,444 pamoja na km² 7925 za maji ya Ziwa Viktoria zikiwa pamoja na visiwa 20.
Wilaya hiyo ina majimbo mawili ya uchaguzi ambapo kuna jimbo la Muleba Kusini lenye kata 28 ambapo Mbunge wake ni Dkt. Oscar Kikoyo na Muleba Kaskazini lenye kata 15 ambapo mbunge wake ni Adonis Bitegeko.
Wakazi
Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 540,310[2] na katika ile ya mwaka 2022 walihesabiwa 637,659 [3].
Marejeo
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa" (PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 2018-08-05. Iliwekwa mnamo 2018-02-01.
- ↑ Sensa ya 2012, Kagera - Muleba-District-Council
- ↑ https://www.nbs.go.tz
| Kata za Wilaya ya Muleba - Mkoa wa Kagera - Tanzania |
||
|---|---|---|
|
Biirabo | Bisheke | Buganguzi | Buhangaza | Bulyakashaju | Bumbire | Bureza | Burungura | Goziba | Gwanseli | Ibuga | Ijumbi | Ikondo | Ikuza | Izigo | Kabirizi | Kagoma | Kamachumu | Karambi | Kasharunga | Kashasha | Katoke | Kerebe | Kibanga | Kikuku | Kimwani | Kishanda | Kyebitembe | Mafumbo | Magata Karutanga | Mayondwe | Mazinga | Mubunda | Muhutwe | Muleba | Mushabago | Ngenge | Nshamba | Nyakabango | Nyakatanga | Ruhanga | Rulanda | Rutoro | ||
| Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Muleba kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |