Agabo
Agabo (kwa Kigiriki Ἄγαβος, Agabos) alikuwa mmojawapo kati ya Wakristo wa kwanza kati ya Palestina na Siria.
Anatajwa mara mbili na kitabu cha Matendo ya Mitume kama nabii aliyeongozwa na Roho Mtakatifu[1].
Agabo anaheshimiwa kama mtakatifu na madhehebu mbalimbali ya Ukristo.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Februari, 8 Machi au 8 Aprili[2][3].
Habari zake
[hariri | hariri chanzo]Kadiri ya Mdo 11:27-28, alikuwa mmoja wa manabii waliofika Antiokia kutoka Yerusalemu na alitabiri njaa kali iliyotokea duniani kote wakati wa kaisari Klaudio.
Kadiri ya Mdo 21:10-12, miaka mingi baadaye (58 hivi BK), Agabo alikutana na Mtume Paulo huko Kaisarea Maritima akamtabiria atakavyokamatwa mapema na kuteswa na watu wa mataifa.
Kadiri ya mapokeo alikuwa mmojawapo kati ya wanafunzi 70/72 wa Yesu na alifia dini huko Antiokia, lakini hakuna hakika yoyote[4].
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- "Agabus" at the Catholic Encyclopedia. Retrieved January 10, 2006.
| Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Agabo kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |