Gamma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Γ)
Alfabeti ya Kigiriki
Herufi za kawaida
Α α Alfa 1 Ν ν Ni 50
Β β Beta 2 Ξ ξ Ksi 60
Γ γ Gamma 3 Ο ο Omikron 70
Δ δ Delta 4 Π π Pi 80
Ε ε Epsilon 5 Ρ ρ Rho 100
Ζ ζ Dzeta 7 Σ σ ς Sigma 200
Η η Eta 8 Τ τ Tau 300
Θ θ Theta 9 Υ υ Ipsilon 400
Ι ι Iota 10 Φ φ Phi 500
Κ κ Kappa 20 Χ χ Khi 600
Λλ Lambda 30 Ψ ψ Psi 700
Μ μ Mi 40 Ω ω Omega 800
Herufi za kihistoria1
Digamma 6 San 90
Stigma 6 Sho 90
Heta 8 Koppa 90
Sampi 900
1 Viungo vya Nje:
Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje

Gamma ni herufi ya tatu katika Alfabeti ya Kigiriki. Inaandikwa Γ (herufi kubwa ya mwanzo) au γ (herufi ndogo ya kawaida). Zamani ilikuwa pia alama kwa namba 3.

Asili ya gamma ni herufi ya Kifinisia ya gimel (tazama makala ya G). Matamshi yake ni kama G ya Kiswahili.

Jinsi ilivyo kawaida na herufi mbalimbali za kigiriki inatumiwa kama kifupi kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hesabu na fizikia. Imejulikana hasa kama jina la pembe ya tatu katika pembetatu.

Katika fizikia gamma ni alama kwa fotoni hasa mnururisho mkali aina miali ya gamma.

Katika astronomia inatumiwa kuanza hesabu ya nyota katika kundinyota. Katika mfumo wa Bayer inataja nyota angavu ya tatu katika kundinyota fulani.