Bujumbura

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Jiji la Bujumbura
Skyline ya Jiji la Bujumbura
Nchi Burundi
Mkoa Bujumbura Mairie
Idadi ya wakazi
 - Mji 300 000
Website: www.villedebujumbura.org
Bujumbura kando la ziwa Tanganyika

Bujumbura, ni Mji Mkuu wa Burundi unaokadiriwa kuwa na idadi ya wakazi 300,000. Mji huu upo kaskazini mashariki mwa Ziwa Tanganyika, na ni mji mkubwa zaidi Burundi, kitovu cha mawasiliano na uchumi nchini humo. Bujumbura ni mji pekee Burundi ambao una bandari ya kupakia mali na bidhaa mbalimbali za kuuza nje. Bidhaa kama kahawa, pamba, ngozi, na madini ya stani. Kwa kijiographia Bujumbura iko 3°22'34" Kusini, 29°21'36" Mashariki (-3.3761111, 29.36) [1].

Bujumbura ilipanuka toka ilipokuwa kijiji kidogo kilichokuwa kambi ya Jeshi ya Wajerumani. Eneo hii iliitwa Afrika ya Mashariki ya Ujerumani mwaka wa 1889. Lakini, baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Bujumbura ilichukuliwa na Ubeljiji ambapo Ligi ya Kimataifa ilisimamia Ruanda-Urundi. Jina la mji likabadilishwa kutoka Usumbura hadi Bujumbura Burundi ilipopata uhuru, mwaka wa 1962. Bujumbura ni mji ambao umeshuhudia vita vya ukabila kati ya Wahutu na Watutsi kwa kung'ang'ania Uongozi wa Burundi.

Kati ya mji huu kuna majengo ni yale ya kikoloni na pia kuna soko, uwanja wa taifa, mskiti mkubwa na kathidro. Pia kuna Jumba la Makumbusho ambalo linaitwa jumba la makumbusho ya maisha na jumba la makumbusho ya Jiologia. Mambo mengine ya kuchangamsha ni kama Hifadhi ya Rusizi, na Kiamba hapo Mugere, ambapo panasemekana kwamba David Livingstone na Henry Stanley walikutana. (Lakini watu wengi wasema walikutana Ujiji), Kigoma, nchini Tanzania ambapo panasemekana ni mwanzo wa mto ulio unaosemekana kuwa hapo ndio mwanzo wa Mto Nile.

[hariri] Viungo vya nje

Africa satellite plane.jpg Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bujumbura kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: