Yosefu wa Studion

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Yosefu wa Studion (Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 760 hivi – Thessalia, Ugiriki, 15 Julai 832) alikuwa mmonaki kama familia yake yote, pia mtunzi wa tenzi na matini mengine ya liturujia[1], halafu askofu mkuu wa Thesalonike kuanzia mwaka 806/807 hadi alipoondolewa madarakani.

Anakumbukwa pia kwa kumlaumu kaisari na kwa kutetea kwa nguvu picha takatifu, bila kujali kwamba msimamo wake ulimvutia tena na tena dhuluma pamoja na kaka yake Theodoro wa Studion hata akafariki uhamishoni kwa njaa[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Julai[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Joseph is known as a spiritual songwriter. He composed the triodia and stichera of the Lenten Triodion, a canon for the Sunday of the Prodigal Son's Week and other hymns. He wrote several sermons for feastdays, of which the best known is the Sermon on the Exaltation of the Precious and Life-Giving Cross of the Lord ("Λόγος είς τόν τίμιον καί ζωοποιόν Σταυρόν").
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/62780
  3. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.