Yosefu wa Anchieta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Yosefu wa Anchieta.

Yosefu wa Anchieta (kwa Kihispania: José de Anchieta y Díaz de Clavijo, S.J.; San Cristóbal de La Laguna, Tenerife, Visiwa vya Kanari, Hispania, 19 Machi 1534Reritiba, Brazil, 9 Juni 1597) tangu ujanani alikuwa mmisionari katika koloni la Brazil katika karne ya 16[1].

Pamoja na mwenzake Manuel da Nóbrega alisaidia Waindio wengi kuingia Ukristo[2] na kuwapatanisha na wakoloni Wareno.

Anchieta ni kati ya waanzilishi wa jiji la São Paulo (1554) na Rio de Janeiro (1565) lakini pia wa fasihi ya Kibrazil[3].

Alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri tarehe 22 Juni 1980, halafu Papa Fransisko akamtangaza mtakatifu tarehe 3 Aprili 2014[4][5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/56550
  2. Anchieta is commonly known as "the Apostle of Brazil".
  3. With his book Arte de gramática da língua mais usada na costa do Brasil, Anchieta became the first person to provide an orthography to the Old Tupi language most commonly spoken by the indigenous people of Brazil.
  4. El Papa convierte hoy al Padre Anchieta en santo
  5. José de Anchieta será o terceiro santo do Brasil
  6. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Helen Dominian, Apostle of Brazil: The Biography of Padre José Achieta, S.J. (1534–1597) (NY: Exposition Press, 1958)
  • Jorge de Lima, Anchieta (Rio de Janeiro: Civilisaçao Brisiliera, 1934)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.