Nenda kwa yaliyomo

Watrinitari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lebo ya shirika.
Juan Carreño de Miranda. Kuanzishwa kwa shirika la Utatu mtakatifu (Misa ya Yohane wa Matha).

Shirika la Utatu Mtakatifu (kifupi Watrinitari, kutokana na neno la Kilatini Trinitas, maana yake Utatu) ni utawa wa Kanisa Katoliki ambao ulianzishwa kwenye eneo la Cerfroid, kilometa 80 hivi kaskazini mashariki kwa Paris (Ufaransa), mwishoni mwa karne ya 12.

Mwanzilishi wake alikuwa Yohane wa Matha, ambaye alikubaliwa na Papa Innocent III kwa waraka Operante divine dispositionis clementia, uliotolewa tarehe 17 Desemba 1198.

Lengo lilikuwa kuheshimu fumbo la Utatu mtakatifu pamoja na kukomboa Wakristo waliotekwa utumwani katika vita vya msalaba.

Leo shirika lina nyumba katika nchi mbalimbali za Ulaya na Amerika, halafu Madagascar, Misri, India, Korea na Philippines.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
    • Text is from www.trinitarianhistory.org (2000), written by Fr. Joseph Gross, who is a member of the Order of the Holy Trinity and a scholar. He has done much research and study as well as writing extensively on the subject of the Order. (though it seems it has been changed now in places by others.

    Viungo vya nje

    [hariri | hariri chanzo]
    Wikimedia Commons ina media kuhusu:
    Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
    Je, unajua kitu kuhusu Watrinitari kama historia yake au maelezo zaidi?
    Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
    Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.