Songambele (Kongwa)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa matumizi mengine za jina hili angalia Songambele

Songambele ni kata ya Wilaya ya Kongwa katika Mkoa wa Dodoma, Tanzania yenye postikodi namba 41518[1].

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 23,342 [2]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na watu wapatao 17,712 waishio humo.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Ni miongoni mwa kata ambazo zinafanya vizuri katika kulima na kufuga. Mazao ambayo yanastawi kwa wingi ni karanga, mahindi, uwele, alizeti na mtama. Wakazi wapo mstari wa mbele katika kilimo cha umwagiliaji; kwa mfano kupitia umwagiliaji wanalima mbogamboga na baadhi mazao ya chakula kama vile mahindi.

Pia ni sehemu nzuri kwa kufanya biashara. Kuna wafanyabiashara wadogowadogo kama wauzaji nyama, nafaka na mifugo; pia lipo gulio la kila wiki, kuna maduka ya jumla na rejareja, n.k.

Ukiwa Songambele unaweza kufanya uwekezaji katika kilimo, biashara, kuanzisha shule za awali, kutoa huduma za afya kama vile maduka ya dawa na hospitali.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2020-03-21. Iliwekwa mnamo 2017-11-01.
  2. https://www.nbs.go.tz
Kata za Wilaya ya Kongwa - Mkoa wa Dodoma - Tanzania

Chamkoroma | Chitego | Chiwe | Hogoro | Iduo | Kibaigwa | Kongwa | Lenjulu | Makawa | Matongoro | Mkoka | Mlali | Mtanana | Ng'humbi | Ngomai | Njoge | Pandambili | Sagara | Sejeli | Songambele | Ugogoni | Zoissa


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Dodoma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Songambele (Kongwa) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.