Cesidio Giacomantonio

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Sesidio Giacomantonio)
Picha halisi ya Mt. Cesidio wa Fossa kabla hajaondoka Italia kwenda China.

Cesidio Giacomantonio (Fossa, Italia, 30 Agosti 1873 - Hengzhou, 4 Julai 1900) alikuwa padri wa shirika la Ndugu Wadogo Wareformati aliyefia dini China alipokuwa mmisionari kwa kupigwa mawe na hatimaye kuchomwa moto akiwa hai ndani ya blanketi lililotiwa petroli alipokuwa anajaribu kuokoa Ekaristi wakati wa Uasi wa Waboksa[1].

Anaheshimiwa na Kanisa hilo kama mtakatifu mfiadini tangu tarehe 1 Oktoba 2000, alipotangazwa na Papa Yohane Paulo II pamoja na wenzake 119 maarufu kama wafiadini wa China.

Sikukuu yao huadhimishwa kwa pamoja kila mwaka tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe tarehe 4 Julai[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/91737
  2. Martyrologium Romanum
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.